Waliobaki, walikimbilia katika muji wa Afeki. Kule, kuta za muji ziliwaangukia na kuwaua watu elfu makumi mbili na saba waliobakia. Beni-Hadadi vilevile alikimbia na kujificha katika chumba fulani cha ndani, katika muji.
Yehu aliporudi kwa wenzake, mumoja wao alimwuliza: “Kuna shida yoyote? Mwenda-wazimu huyu alitaka nini kwako?” Yehu akawajibu: “Si munamujua yeye na namna yake ya kusema?”
Yehu mwana wa Yosafati, ambaye vilevile alikuwa mujukuu wa Nimusi, alifanya mupango wa kuasi Yoramu. Yoramu na watu wote wa Israeli walikuwa Ramoti-Gileadi kwa kulinda zamu juu ya mufalme Hazaeli wa Aramu.
Kwa mara ingine tena mulinzi akasema: “Mujumbe amewafikia lakini harudi.” Halafu akaongeza: “Uendeshaji wa gari ni kama wa Yehu mwana wa Nimusi, kwa sababu yeye anaendesha mbiombio.”