Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Wafalme 8:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Hazaeli akapakia zawadi za kila aina ya mazao ya Damasiki kipimo cha mizigo ya ngamia makumi ine na kumupelekea Elisha. Alipofika kwa Elisha alimwambia: “Mutumishi wako, Beni-Hadadi, mufalme wa Aramu amenituma kwako. Yeye anauliza: ‘Nitapona ugonjwa huu?’ ”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Wafalme 8:9
13 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Umupelekee mikate kumi, na maandazi, na chupa moja ya asali. Yeye atakuambia yatakayomupata mutoto wetu.”


Halafu mufalme Asa akatwaa feza na zahabu yote iliyobaki katika hazina ya nyumba ya Yawe na katika hazina ya nyumba ya kifalme, akawapa watumishi wake, akawatuma Damasiki kwa Beni-Hadadi mwana wa Taburimoni, mujukuu wa Hesioni, mufalme wa Aramu, akasema:


Yawe akamwambia: “Urudie kwa kupitia njia ya jangwa mpaka Damasiki. Utakapofika, umupakae Hazaeli mafuta akuwe mufalme wa Aramu.


Mufalme Ahazia alipokuwa Samaria alianguka kutoka chumba kilichokuwa juu ya paa ya nyumba yake, akaumia vibaya. Kwa hiyo akawatuma wajumbe, akawaambia: “Muende kwa Bali-Zebubu, mungu wa muji wa Ekuroni, mumwulize kama nitapona ugonjwa huu.”


Nabii Elisha alipata ugonjwa ambao ulimwua. Alipokuwa karibu kufa, mufalme Yehoasi wa Israeli alimutembelea. Alipomufikia Elisha, akalia, akisema: “Baba yangu, baba yangu! Ulikuwa wa lazima kuliko magari ya Israeli na wapanda-farasi wake!”


Basi Ahazi akatuma watu kwa mufalme Tigilati-Pileseri wa Asuria wakiwa na ujumbe huu: “Mimi ni mutumishi wako mwaminifu. Ukuje uniokoe kutoka kwa wafalme wa Aramu na Israeli ambao wananishambulia.”


Watumishi wake wakamwendea na kumwambia: “Baba yetu, kama nabii angekuambia ufanye jambo fulani gumu, haungelifanya? Sasa, aliyokuambia tu ni: ‘Ujioshe, kusudi upone!’ ”


Mufalme wa Aramu akamwambia: “Twaa barua hii umupelekee mufalme wa Israeli.” Hivyo Namani akaondoka, akipeleka vikoroti elfu makumi tatu vya feza, vikoroti elfu sita vya zahabu na nguo kumi za sikukuu.


Mufalme wa Israeli alipowaona Waaramu, alimwuliza Elisha: “Niwaue?”


wakati wa kutafuta na wakati wa kupoteza, wakati wa kuchunga na wakati wa kutupa,


Lakini sikutaka kufanya kitu chochote pasipo shauri lako. Wala sikutaka kukulazimisha unitendee mema; lakini ningetaka uyatende kwa mapenzi yako mwenyewe.


Ukiwauliza, watakuambia. Sasa ninakuomba vijana wangu hawa wapate kukubaliwa mbele yako, maana tumefika wakati wa sikukuu. Tafazali uwapatie kitu chochote unachokuwa nacho watumishi wako hawa nami mwana wako Daudi.’ ”


Saulo akamwuliza: “Lakini tukimwendea, tutamupa nini? Angalia, mikate katika mifuko yetu imekwisha na hatuna chochote cha kumupa yule mutu wa Mungu. Tuna nini?”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ