Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Wafalme 8:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Kisha Elisha alikwenda Damasiki. Wakati ule mufalme Beni-Hadadi alikuwa mugonjwa na alipoambiwa kwamba Elisha alikuwa Damasiki,

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Wafalme 8:7
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kule, akagawanya jeshi lake katika makundi. Usiku, akawashambulia waadui zake, akawashinda na kuwafukuza mpaka Hoba, upande wa kaskazini wa Damasiki.


Nyuma ya Daudi kufanya mauaji kule Zoba, Resoni alikusanya watu, naye mwenyewe akakuwa kiongozi wao. Basi, wakaenda Damasiki, wakakaa kule na kumufanya Resoni mufalme wa Damasiki.


Siku moja Yeroboamu alikuwa akisimama pembeni ya mazabahu kusudi afukize ubani. Basi, mutu wa Mungu kutoka Yuda akafika pale Beteli na ujumbe wa Yawe.


Halafu mufalme Asa akatwaa feza na zahabu yote iliyobaki katika hazina ya nyumba ya Yawe na katika hazina ya nyumba ya kifalme, akawapa watumishi wake, akawatuma Damasiki kwa Beni-Hadadi mwana wa Taburimoni, mujukuu wa Hesioni, mufalme wa Aramu, akasema:


Beni-Hadadi mufalme wa Aramu alikusanya waaskari wake wote. Aliungwa mukono na wafalme wengine makumi tatu na wawili pamoja na farasi na magari yao ya vita. Aliuendea muji wa Samaria akauzunguka na kuushambulia.


Kisha, Beni-Hadadi akamwambia: “Miji yote ambayo baba yangu alimunyanganya baba yako, nitakurudishia. Unaweza kuanzisha masoko kule Damasiki kama vile baba yangu alivyofanya kule Samaria.” Ahabu akajibu: “Nitakuachilia kwa masharti hayo.” Hapo, akafanya mapatano naye na kumwacha huru.


Mufalme Ahazia alipokuwa Samaria alianguka kutoka chumba kilichokuwa juu ya paa ya nyumba yake, akaumia vibaya. Kwa hiyo akawatuma wajumbe, akawaambia: “Muende kwa Bali-Zebubu, mungu wa muji wa Ekuroni, mumwulize kama nitapona ugonjwa huu.”


Wale wanafunzi wa manabii kutoka Yeriko walipomwona, walisema: “Roho wa Elia yuko kwa Elisha.” Basi, wakaenda kumupokea, wakainama mbele yake kwa heshima.


Gehazi, mutumishi wa Elisha mutu wa Mungu, akasema: “Bwana wangu amemwachilia Namani wa Aramu aende bila kupokea chochote alicholeta. Kama vile Yawe anavyoishi, nitamufuata kusudi nipate kitu kutoka kwake.”


Mumoja wao akajibu: “Hakuna anayekuwa upande wake, ee mufalme. Anayefanya vile ni Elisha, nabii anayekuwa kule Israeli. Yeye anamwambia mufalme wa Israeli mambo yote unayosema hata ukiwa katika chumba chako cha kulala.”


Nyuma ya hayo, mufalme Beni-Hadadi wa Aramu akakusanya waaskari wake wote akatoka na kuuzunguka muji wa Samaria.


Mufalme alipomwuliza mwanamuke yule, yeye alimwelezea. Mufalme akamwita mukubwa wa waaskari wake na kumwamuru amurudishie mwanamuke yule mali yake yote, pamoja na mapato yote ya mashamba yake katika muda ule wote wa miaka saba.


Maana muji mukubwa wa Aramu ni Damasiki, na huyo Resini ni mukubwa wa Damasiki tu. Muji mukubwa wa Efuraimu ni Samaria, na mwana wa Remalia ni mukubwa wa Samaria tu. Katika miaka makumi sita na mitano utawala wa Efuraimu utavunjwa; Efuraimu halitakuwa taifa tena. Kama hautaamini, hautaimarika.


Kama ukiamua kubaki, basi rudi kwa Gedalia mwana wa Ahikamu, mujukuu wa Safanu, ambaye mufalme wa Babeli amemusimika kuwa mutawala wa miji yote ya Yuda, ukae naye kati ya wanainchi wengine. Kama sivyo, kwenda kwenye unaona unastahili kwenda. Basi, mukubwa wa walinzi akamupa Yeremia vyakula na zawadi, kisha akamwacha ajiendee.


Kwa kuwa hawakuwapata, wakamupeleka Yasoni pamoja na wandugu waamini wengine mbele ya wakubwa wa muji. Wakalalamika wakisema: “Watu hawa walifanya fujo fasi zote na sasa wamefika huku.


Hii ndiyo baraka ambayo Musa, mutu wa Mungu aliwatakia Waisraeli mbele ya kufa kwake. Alisema hivi:


Watu wa Gaza walipoambiwa kwamba Samusoni yuko kule, wakalizunguka eneo hilo na kumuvizia kwenye mulango wa muji usiku kucha. Wakakaa kimya kule kwenye mulango usiku wote wakifikiri kwamba wanaweza kungojea mpaka mapambazuko wapate kumwua.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ