Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Wafalme 8:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Gehazi alipokuwa anamwambia mufalme jinsi Elisha alivyofufua mutu aliyekufa, mwanamuke yule alitoa ombi lake kwa mufalme. Gehazi akasema: “Ee mufalme; huyu ndiye mwanamuke ambaye Elisha alimufufua mwana wake!”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Wafalme 8:5
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Elisha akasimama na kutembeatembea ndani ya chumba, kisha akarudi na kujilaza tena juu ya mutoto. Mutoto akapiga chafya mara saba, halafu akafungua macho.


Basi kufuatana na mambo hayo, tuseme nini zaidi? Mungu akiwa upande wetu, ni nani anayeweza kupingana nasi?


Tena, nimeona kitu kimoja hapa chini ya jua, kwamba wenye kukimbia mbio hawashindi katika mashindano ya kukimbia, wala wenye nguvu hawashindi vita, wenye hekima hawapati chakula, wenye akili hawatajiriki, wala wenye ujuzi hawapandi vyeo. Lakini wakati wa bahati unawapata wote pamoja.


Mutu anaweza kufanya mipango yake, lakini Yawe anaongoza hatua zake.


Wimbo wa sifa wa Daudi. Nitakutukuza, ee Mungu wangu na mufalme wangu; nitalitukuza jina lako kwa milele na milele.


Basi, muke wake Zeresi na warafiki zake wakamushauria hivi: “Kwa nini asitengenezewe muti wa kutundikia, wenye urefu wa metre makumi mbili na mbili? Kesho asubui, unaweza kuzungumuza na mufalme kusudi Mordekayi auawe juu yake, kisha uende ukule karamu na mufalme kwa furaha.” Wazo hilo lilimufurahisha Hamani, naye akatengeneza muti ule.


Siku moja mufalme wa Israeli alipokuwa anatembea juu ya ukuta wa muji, alisikia mwanamuke mumoja akimwita: “Unisaidie, ee bwana wangu mufalme!”


Mumoja wao akajibu: “Hakuna anayekuwa upande wake, ee mufalme. Anayefanya vile ni Elisha, nabii anayekuwa kule Israeli. Yeye anamwambia mufalme wa Israeli mambo yote unayosema hata ukiwa katika chumba chako cha kulala.”


Saulo alitambua sauti ya Daudi, akamwuliza: “Hiyo ni sauti yako mwana wangu Daudi?” Daudi akamujibu: “Bwana wangu mufalme, ni sauti yangu.”


Basi Ruta akaenda katika shamba, akawafuata wavunaji naye akiyaokota masuke waliyoyaacha. Na kumbe akajikuta katika shamba la Boazi, yule wa ukoo wa Elimeleki.


Akamwambia mutumishi wake Gehazi: “Umwite yule mama Musunami.” Alipomwita akakuja na kusimama mbele yake.


Mufalme alipomwuliza mwanamuke yule, yeye alimwelezea. Mufalme akamwita mukubwa wa waaskari wake na kumwamuru amurudishie mwanamuke yule mali yake yote, pamoja na mapato yote ya mashamba yake katika muda ule wote wa miaka saba.


Beni-Hadadi mufalme wa Aramu alikusanya waaskari wake wote. Aliungwa mukono na wafalme wengine makumi tatu na wawili pamoja na farasi na magari yao ya vita. Aliuendea muji wa Samaria akauzunguka na kuushambulia.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ