Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Wafalme 8:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Akamukuta mufalme akiongea na Gehazi, akisema: “Tafazali, uniambie miujiza ambayo inatendwa na Elisha.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Wafalme 8:4
24 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Akayapiga maji kwa nguo ya Elia akisema: “Yuko wapi Yawe, Mungu wa Elia?” Alipopiga maji, yakagawanyika sehemu mbili, naye akavuka mpaka ngambo.


Elisha aligeuka, akawaangalia na kuwalaani kwa jina la Yawe. Dubu wawili wakatoka katika pori, wakawararua vijana makumi ine na wawili kati yao.


Akamwambia mutumishi wake Gehazi: “Umwite yule mama Musunami.” Alipomwita akakuja na kusimama mbele yake.


Basi, akaondoka, akaenda mpaka kwenye mulima Karmeli kule mutu wa Mungu alipokuwa. Mutu wa Mungu alipomwona akikuja, akamwambia Gehazi mutumishi wake: “Angalia, ninamwona Musunami akikuja.


Basi, Namani akateremuka kwenye muto Yordani akajitumbukiza mule mara saba, kama alivyoagizwa na Elisha mutu wa Mungu, naye akapona kabisa. Ngozi yake ikakuwa laini na yenye afya kama ya mutoto mudogo.


Halafu akatuma mujumbe kwenda kumuleta Elisha. Wakati uleule, Elisha alikuwa ndani ya nyumba pamoja na wazee waliomutembelea. Mbele ya kufika kwa mujumbe wa mufalme, Elisha akawaambia wazee: “Yule mwuaji amemutuma mutu kuja kunikata kichwa! Atakapofika hapa, mufunge mulango, wala musimuruhusu aingie. Vilevile bwana wake anamufuata nyuma.”


Elisha akauliza: “Liliangukia wapi?” Mutu huyo akamwonyesha. Elisha akakata kijiti na kukitupa ndani ya maji na palepale shoka likaelea juu ya maji.


Elisha akamujibu: “Sikiliza neno la Yawe: Kesho kwa wakati kama huu, humu Samaria kilo tatu za unga bora wa ngano zitanunuliwa kwa kipande kimoja cha feza, na kilo sita za shayiri kwa kipande kimoja cha feza.”


Hivyo, wakaondoka katika kambi ya Waaramu na kuwaita walinda milango ya muji na kuwaambia: “Tulikwenda katika kambi ya Waaramu na hatukuweza kumwona wala kumusikia mutu yeyote. Farasi na punda wangali wanafungwa, na mahema yako kama walivyoyaacha.”


Kulikuwa watu wane wenye ugonjwa wa ukoma waliokuwa inje ya milango ya muji wa Samaria ambao walisemezana, wao kwa wao: “Mbona tunakaa hapa tukikufa na njaa?


Miaka saba ilipokwisha, alitoka katika inchi ya Wafilistini akarudi Israeli na kwenda kwa mufalme kuomba arudishiwe nyumba yake na shamba lake.


Kisha akawatuma Betelehemu, akiwaambia: “Mwende mupeleleze habari kamili za mutoto yule. Nanyi mutakapomwona munijulishe kusudi mimi vilevile niende kumwabudu.”


Herode alipomwona Yesu, akafurahi sana. Tangu siku nyingi alitamani kumwona kwa sababu alikuwa amesikia habari zake, naye alitumaini kuona kitambulisho kutoka kwake.


Lakini Herode alisema: “Mimi nimeamuru Yoane akatwe kichwa. Basi huyu ninayesikia habari zake ni nani?” Naye akatafuta namna ya kumwona Yesu.


Naye akawajibu: “Nimekwisha kuwaelezea lakini hamupendi kusikia. Kwa sababu gani munataka niwaambie tena? Ninyi vilevile munataka kuwa wanafunzi wake?”


Nyuma ya siku chache, liwali Feliki akakuja pamoja na muke wake Drusila, aliyekuwa Muyuda. Akaamuru wamwite Paulo, naye akasikiliza maneno aliyosema juu ya kumwamini Kristo Yesu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ