Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Wafalme 8:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Miaka saba ilipokwisha, alitoka katika inchi ya Wafilistini akarudi Israeli na kwenda kwa mufalme kuomba arudishiwe nyumba yake na shamba lake.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Wafalme 8:3
10 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Huyo mwanamuke kutoka Tekoa akaenda kwa mufalme, akainama uso mpaka chini mbele ya mufalme, akamwambia: “Ee mufalme, unisaidie.”


Naye Elisha akamwambia Gehazi: “Umwambie, tumeona jinsi alivyotushugulikia; sasa anataka tumutendee jambo gani? Angependa aombewe lolote kwa mufalme au kwa jemadari wa waaskari?” Mama Musunami akamujibu: “Mimi ninaishi kati ya watu wangu.”


Siku moja mufalme wa Israeli alipokuwa anatembea juu ya ukuta wa muji, alisikia mwanamuke mumoja akimwita: “Unisaidie, ee bwana wangu mufalme!”


Yule mwanamuke akaondoka, akafanya kama vile mutu wa Mungu alivyosema. Akaenda pamoja na jamaa yake na kukaa kama mugeni katika inchi ya Wafilistini kwa miaka saba.


Akamukuta mufalme akiongea na Gehazi, akisema: “Tafazali, uniambie miujiza ambayo inatendwa na Elisha.”


Mufalme alipomwuliza mwanamuke yule, yeye alimwelezea. Mufalme akamwita mukubwa wa waaskari wake na kumwamuru amurudishie mwanamuke yule mali yake yote, pamoja na mapato yote ya mashamba yake katika muda ule wote wa miaka saba.


Aliwapatia haki wamasikini na wakosefu, na mambo yake yaliendeka vizuri. Si hivi ndivyo kunijua mimi? –Ni ujumbe wa Yawe.–


Akaondoka pahali pale alipoishi pamoja na wakwe zake, wakashika njia ya kurudi Yuda.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ