Naye Elisha akamwambia Gehazi: “Umwambie, tumeona jinsi alivyotushugulikia; sasa anataka tumutendee jambo gani? Angependa aombewe lolote kwa mufalme au kwa jemadari wa waaskari?” Mama Musunami akamujibu: “Mimi ninaishi kati ya watu wangu.”
Yule mwanamuke akaondoka, akafanya kama vile mutu wa Mungu alivyosema. Akaenda pamoja na jamaa yake na kukaa kama mugeni katika inchi ya Wafilistini kwa miaka saba.
Mufalme alipomwuliza mwanamuke yule, yeye alimwelezea. Mufalme akamwita mukubwa wa waaskari wake na kumwamuru amurudishie mwanamuke yule mali yake yote, pamoja na mapato yote ya mashamba yake katika muda ule wote wa miaka saba.