Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Wafalme 7:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Lakini wakaambiana: “Tunalofanya si sawa! Hii ni habari njema tunayokuwa nayo leo, na ikiwa tutangoja mpaka asubui, bila shaka tutaazibiwa. Tuende mara moja tuwaambie watu wa nyumba ya mufalme!”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Wafalme 7:9
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Namani alipopata habari hii, akaenda kwa mufalme na kumwelezea habari za mutoto yule.


Hivyo, wakaondoka katika kambi ya Waaramu na kuwaita walinda milango ya muji na kuwaambia: “Tulikwenda katika kambi ya Waaramu na hatukuweza kumwona wala kumusikia mutu yeyote. Farasi na punda wangali wanafungwa, na mahema yako kama walivyoyaacha.”


Kulikuwa watu wane wenye ugonjwa wa ukoma waliokuwa inje ya milango ya muji wa Samaria ambao walisemezana, wao kwa wao: “Mbona tunakaa hapa tukikufa na njaa?


Maana Yawe alikuwa amewasikilizisha waaskari wa Waaramu sauti kama ya kundi kubwa lililokuwa na magari na farasi. Waaramu wakazani kwamba mufalme wa Israeli amelipa waaskari wa Wahiti na Wamisri kuja kuwashambulia.


Wale watu wane wenye ukoma walipofika pembeni ya kambi, waliingia ndani ya hema moja, wakakula na kunywa vile walivyopata mule, wakatwaa feza, zahabu na nguo, wakaenda kuzificha. Wakaingia katika hema ingine na kufanya vivyo hivyo.


maana mutu wa haki anaanguka mara nyingi naye anainuka tena, lakini mutu mwovu anaangamizwa na hasara.


Mimi ni yule wa kwanza. Nilitangaza kwa Sayuni, nikapeleka Yerusalema mujumbe wa habari njema.


Ni furaha kabisa! Mujumbe anatokea kwenye mulima. Anatangaza habari njema za amani, heri, na ukombozi. Anauambia Sayuni: Mungu wako anatawala!


Lakini ninawaonya kwamba musipotimiza ahadi yenu, mutakuwa mumemutendea Yawe zambi; mujue kwa hakika kwamba mutaazibiwa.


Lakini malaika akawaambia: “Musiogope, kwa sababu ninawaletea Habari Njema itakayofurahisha sana watu wote.


Kila mutu asitafute faida yake mwenyewe, lakini atafute faida ya watu wengine.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ