Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Wafalme 7:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Maana Yawe alikuwa amewasikilizisha waaskari wa Waaramu sauti kama ya kundi kubwa lililokuwa na magari na farasi. Waaramu wakazani kwamba mufalme wa Israeli amelipa waaskari wa Wahiti na Wamisri kuja kuwashambulia.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Wafalme 7:6
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Waamoni walipoona kwamba wamemuchukiza Daudi, walijilipia waaskari wa miguu wa Waaramu elfu makumi mbili kutoka Beti-Rehobu na Zoba, waaskari elfu kumi na mbili kutoka Tobu, na mufalme Maka akiwa na waaskari elfu moja.


Na mara moja mutakaposikia vishindo vya miguu kwenye vilele vya miforosadi hiyo, halafu ujipe moyo maana nitakuwa nimetoka kwa kukutangulia kuwapiga waaskari wa Wafilistini.”


Gari moja liliweza kununuliwa kule Misri kwa feza inayopita kilo saba, na farasi mumoja aliweza kununuliwa kwa feza kilo mbili. Wachuuzi wa mufalme walisafirisha magari na farasi hao na kuwauzishia wafalme wote wa Wahiti na wa Waaramu.


Kila mumoja wao akamwua adui mumoja. Watu wa Aramu wakakimbia, nao waaskari wa Israeli wakawafuatilia. Lakini Beni-Hadadi mufalme wa Aramu akapanda juu ya farasi, akatoroka na sehemu ya waaskari wapanda-farasi.


Sikia, nitamufanya mufalme asikie uvumi, halafu atarudi katika inchi yake, na kule nitamufanya auawe kwa upanga.’ ”


Hivyo, giza lilipoanza kuingia, wakaenda kwa kambi ya Waaramu, lakini walipofika kule, hakukuwa mutu.


Sauti za vitisho zitamupigia kelele katika masikio. Anapozani amestawi, mwangamizi atamushambulia.


Hapo watashikwa na hofu, maana Mungu ni pamoja na watu wa haki.


Ole kwao wale wanaokwenda Misri kuomba musaada! Wanategemea farasi, wanategemea wingi wa magari ya vita na nguvu za waaskari wao wapanda-farasi. Lakini hawamutegemei Mutakatifu wa Israeli, wala hawamwombi Yawe shauri!


Hata kama munategemea Misri kupata magari ya vita na waaskari wapanda-farasi, hamuwezi kumurudisha nyuma mutu mumoja wa cheo cha chini sana kati ya watumishi wa bwana wangu.


Hata waaskari wake wa mushahara ni kama wana-ngombe wanono; nao tena wamegeuka, wakakimbia pamoja, wala hawakuweza kuvumilia, kwa maana siku yao ya kuangamizwa imefika, wakati wao wa kuazibiwa umetimia.


Vilipokuwa vinakwenda, nilisikia sauti ya mabawa yao; sauti ya muvumo huo ilikuwa kama ile ya maji mengi, kama sauti ya ngurumo kutoka kwa Mungu wa majeshi, na kama kelele ya jeshi. Viliposimama, vilikunja mabawa yao.


Shindo la mabawa ya makerubi iliweza kusikilika hata kwenye kiwanja cha inje, kama sauti ya Yawe wa majeshi anaposema.


Na juu ya vifua vyao kulikuwa vitu vinavyofanana na ngao za chuma. Na sauti ya mabawa yao ilikuwa kama uvumi wa magari yanayovutwa na farasi wengi wanaokimbia mbio kwenda kwa vita.


Wakasimama kila mumoja kwa nafasi yake kuizunguka kambi. Jeshi lote la waadui likatawanyika nalo likilalamika.


Kulikuwa hofu kubwa katika kambi ya Wafilistini. Wote walianza kufazaika: waaskari katika kambi, watu katika mashamba kwenye kambi, hata na washambulizi. Inchi ilitetemeka. Hofu ilikuwa kubwa sana.


Daudi akamwambia Ahimeleki ambaye alikuwa Muhiti, na Abisai ndugu ya Yoabu (mama yao aliitwa Zeruya): “Nani atakwenda pamoja nami kwenye kambi ya Saulo?” Abisai akamwambia: “Mimi nitakwenda pamoja nawe.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ