Hakuna maana ya kuingia katika muji kwa sababu kule tutakufa. Kwa hiyo kumbe tuende kwenye kambi ya Waaramu. Kama wakituacha kuishi, tutaishi; kama wakituua, tutakufa tu.”
Maana Yawe alikuwa amewasikilizisha waaskari wa Waaramu sauti kama ya kundi kubwa lililokuwa na magari na farasi. Waaramu wakazani kwamba mufalme wa Israeli amelipa waaskari wa Wahiti na Wamisri kuja kuwashambulia.
Naye mutawala wao atabeba muzigo wake juu ya mabega wakati wa usiku, atatoka kupitia ukuta atakaotoboa apate kutoka; atafunika uso wake kusudi asiione inchi kwa macho yake.
Lakini ikiwa mutu huyu ni masikini na hawezi kulipa malipo yake, basi, mutu yule atapelekwa kwa kuhani. Kuhani atapima bei yake kulingana na uwezo wa huyo aliyefanya kiapo.
Mutu mumoja anaweza namna gani kuwashinda watu elfu moja, au watu wawili wanaweza namna gani kuwashinda watu elfu kumi, isipokuwa kama mulinzi wao amewatupa, Yawe amewaacha?
Daudi aliwapiga tangu asubui mpaka siku ya pili magaribi. Hakuna mwanaume yeyote aliyeponyoka isipokuwa vijana mia ine ambao walipanda juu ya ngamia na kukimbia.