Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Wafalme 7:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Jemedari mulinzi wa mufalme akamwambia Elisha: “Hata kama Yawe mwenyewe angefanya madirisha mbinguni, jambo hilo litawezekana?” Elisha akamujibu: “Utaona kwa macho yako mwenyewe, lakini wewe hautakula.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Wafalme 7:2
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Noa alipokuwa na umri wa miaka mia sita, katika siku ya kumi na saba ya mwezi wa pili, siku hiyo chemichemi zote za vilindi vya udongo zikabubujika maji, na madirisha ya mbinguni yakafunguka.


Naye Yawe anisamehe ninapofuatana na mufalme wangu kwenda kuabudu katika hekalu la Rimoni mungu wa Waaramu. Ninapaswa kuinama pamoja naye kwa sababu anaegemea kwenye mukono wangu. Ninaomba Yawe anisamehe!”


Kesho yake, wakaamuka asubui mapema, wakaenda mpaka katika jangwa la Tekoa. Walipokuwa wanaondoka, Yosafati akasimama, akawaambia: “Musikilize, enyi watu wa Yuda na wakaaji wa Yerusalema! Mumwamini Yawe, Mungu wenu, nanyi mutakuwa imara. Muwaaminie manabii wake, nanyi mutashinda.”


Walimujaribu Mungu tena na tena, wakamukasirikisha huyo Mutakatifu wa Israeli.


Kwa hiyo nitamwazibu Semaya wa Nehelamu pamoja na wazao wake. Hakuna hata mumoja wa watu wake atakayebaki muzima na kupata kuona mema nitakayowafanyia watu wangu, kwa sababu amesema maneno ya uasi juu ya Yawe. –Ni ujumbe wa Yawe.


Mulete katika gala yangu zaka yote, kusudi katika nyumba yangu kuwe chakula cha kutosha. Kisha munaweza kunijaribu. Munipime namna hiyo nanyi mutaona kama sitayafungua madirisha ya mbinguni na kuwatiririshia baraka tele.


Nitapata wapi nyama ya kuwakulisha watu hawa wote? Maana wanalia mbele yangu wakisema: Utupatie nyama tukule!


Mungu si mutu, hata aseme uongo, wala si mwanadamu, hata abadilishe nia yake! Ataahidi kitu na asikifanye, au kusema kitu asikitimize?


Tuseme nini basi? Ikiwa wamoja kati yao hawakukuwa waaminifu, jambo hilo litaweza kuonyesha kwamba Mungu ataacha kuwa mwaminifu?


Panda mpaka kwenye kilele cha mulima Pisiga, uangalie vizuri upande wa magaribi, kaskazini, kusini na mashariki, na kuiona inchi hiyo; lakini wewe hautavuka huu muto Yordani.


Kama tunakosa kuwa waaminifu, yeye anabaki mwaminifu. Kwa maana hawezi kujikana yeye mwenyewe.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ