Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Wafalme 7:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Elisha akamujibu: “Sikiliza neno la Yawe: Kesho kwa wakati kama huu, humu Samaria kilo tatu za unga bora wa ngano zitanunuliwa kwa kipande kimoja cha feza, na kilo sita za shayiri kwa kipande kimoja cha feza.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Wafalme 7:1
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kisha Mikaya akasema: “Sasa sikia neno la Yawe: Nilimwona Yawe akiikaa katika kiti chake cha kifalme, na jeshi lote la mbinguni likisimama pembeni yake, upande wake wa kuume na wa kushoto.


Halafu Isaya akamwambia Hezekia: “Sikia neno la Yawe:


Mutu mumoja akatoka Bali-Salisa, akamuletea Elisha mikate makumi mbili iliyotengenezwa kwa shayiri ya malimbuko ya mavuno ya mwaka ule na masuke mabichi ya ngano katika gunia. Elisha akamwagiza Gehazi awape watu wakule.


Matokeo yake ilikuwa njaa kali katika muji wa Samaria. Kichwa cha punda kilinunuliwa kwa vikoroti makumi tatu vya feza, na grama mia moja za mavi ya njiwa zilinunuliwa kwa vikoroti vitano vya feza.


Mbele hata hajamaliza kusema, mufalme akafika, akasema: “Mabaya haya yametoka kwa Yawe! Nitangojea nini tena kutoka kwake?”


Watu wa Samaria wakatoka na kuteka kambi ya Waaramu. Kama vile Yawe alivyosema, kilo tatu za unga bora wa ngano zilinunuliwa kwa kipande kimoja cha feza, na kilo sita za shayiri kwa kipande kimoja cha feza.


Kuna muto ambao maji yake yanafurahisha muji wa Mungu, makao matakatifu ya Mungu Mukubwa.


Musa akawaambia Waisraeli: “Musiogope! Musimame imara! Leo mutaona jinsi Yawe atakavyowaokoa. Maana, hawa Wamisri munaowaona leo, hamutawaona tena.


“Nimesikia manunguniko ya Waisraeli. Basi, uwaambie kwamba wakati wa magaribi watakula nyama na asubui watakula mukate. Hapo ndipo mutakapotambua kwamba mimi ni Yawe, Mungu wenu.”


Tusafiri mwendo wa siku tatu katika jangwa tumutolee Yawe, Mungu wetu, sadaka kama vile atakavyotuamuru.”


Musikilize neno la Yawe, enyi watawala waovu kama wa Sodoma! Musikilize mafundisho ya Mungu wetu, enyi watu waovu kama wa Gomora!


Naye akaniambia: Toa unabii juu ya mifupa hii. Uiambie hivi: Enyi mifupa yenye kukauka, musikilize neno la Yawe.


“Hapa kuna mutoto mumoja anayekuwa na mikate mitano ya shayiri pamoja na samaki mbili. Lakini chakula hiki hakitawafalia kitu watu wengi kama hawa.”


Yoshua akawaambia watu: “Mujitakase kwa sababu kesho Yawe atatenda maajabu kati yenu.”


Nikasikia kitu kama sauti iliyotokea katikati ya vile viumbe vine vya ajabu ikisema: “Kilo moja ya ngano ni mushahara wa siku nzima ya kazi, na kilo tatu ya shayiri ni mushahara wa siku nzima ya kazi, lakini usiharibu mafuta wala divai.”


Wakawaambia wale wajumbe waliorudi kutoka Yabesi: “Muwaambie wakaaji wa Yabesi-Gileadi hivi: kesho, wakati jua linapokuwa kali, mutakuwa mumekombolewa.” Watu wa Yabesi walipopata habari hizo walifurahi sana.


Samweli alimwambia Saulo: “Yawe alinituma kukupakaa mafuta kwa kukusimika kuwa mufalme wa watu wake Waisraeli. Sasa sikiliza maneno ya Yawe.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ