Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Wafalme 6:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Lakini Elisha akamupelekea mufalme wa Israeli habari afanye angalisho na pahali pale, kwa sababu Waaramu walikuwa tayari kupashambulia.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Wafalme 6:9
15 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wakati uleule, nabii mumoja akamwendea Ahabu, mufalme wa Israeli, akamwambia: “Yawe anasema hivi: ‘Unaona wingi wa waaskari hawa? Leo hii nitawatia katika mikono yako, nawe utatambua kwamba mimi ndimi Yawe.’ ”


Halafu, mutu mumoja wa Mungu akamukaribia mufalme wa Israeli, akamwambia: “Yawe anasema hivi: ‘Kwa sababu Waaramu wamesema kwamba mimi Yawe ni Mungu wa milima wala si Mungu wa inchi ya bonde, nitakupa ushindi juu ya kundi hili kubwa, nawe utatambua kwamba mimi ni Yawe.’ ”


Basi, mwanamuke mumoja kati ya wake za wanafunzi wa manabii akamwendea Elisha, akamwambia: “Mutumishi wako, mume wangu amekufa, na kama vile unavyojua, alikuwa mwenye kumwogopa Mungu. Lakini mutu aliyemukopesha feza amekuja kuwatwaa wana wangu wawili wakuwe watumwa wake.”


Alipofika kwenye mulima kwa mutu wa Mungu, akamushika miguu, naye Gehazi akakaribia kusudi amwondoe. Lakini mutu wa Mungu akamwambia: “Umwache, maana ana uchungu mukali, naye Yawe hakunijulisha jambo hilo.”


Akarudi kwa mutu wa Mungu na kumweleza habari hiyo. Naye mutu wa Mungu akamwambia: “Kwenda uuzishe hayo mafuta na kulipa madeni yako, ndipo wewe na wana wako mutaishi kwa kutumia hayo yatakayobaki.”


Basi, mufalme wa Israeli akapeleka waaskari wake karibu na pahali alipoambiwa. Elisha aliendelea kumwonya mufalme naye mufalme alijiweka katika hali ya angalisho. Jambo hilo lilifanyika mara nyingi.


Mumoja wao akajibu: “Hakuna anayekuwa upande wake, ee mufalme. Anayefanya vile ni Elisha, nabii anayekuwa kule Israeli. Yeye anamwambia mufalme wa Israeli mambo yote unayosema hata ukiwa katika chumba chako cha kulala.”


Wakati mumoja kulikuwa vita kati ya Aramu na Israeli. Basi, mufalme wa Aramu akafanya shauri na wakubwa wa waaskari wake juu ya pahali watakapopiga kambi.


Anavunja mipango ya wadanganyifu, matendo yao yasipate mafanikio.


Yawe anavunja mipango ya mataifa, na anabadilisha mawazo yao.


Yawe analinda maarifa lakini anayavuruga maneno ya waovu.


Yawe alinijulisha, nami nikaelewa; Yawe alinijulisha shauri lao baya.


Hakika, Bwana wetu Yawe hafanyi kitu bila kuwafunulia watumishi wake manabii nia yake.


Hizi ni habari za mambo yaliyofunuliwa na Yesu Kristo. Kristo alipata ufunuo huu kutoka kwa Mungu, kusudi awaonyeshe watumishi wake mambo yanayopaswa kutokea kisha kidogo. Kristo alimutuma malaika wake kwa kumujulisha mutumishi wake Yoane mambo yale.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ