Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Wafalme 5:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Mufalme wa Israeli aliposoma barua hii alipasua nguo yake na kusema: “Sababu gani mufalme wa Aramu anataka nimuponyeshe mutu huyu ukoma wake? Anafikiri kwamba mimi ni Mungu anayekuwa na uwezo wa kuua au kufufua? Mufahamu basi, muone kwamba mutu huyu anataka kuniletea ugomvi!”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Wafalme 5:7
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yakobo akamukasirikia Rakeli na kumwambia: “Mimi nimekuwa pahali pa Mungu aliyekuzuia kupata watoto?”


Basi, Rubeni aliporudi kwenye lile shimo, hakumwona Yosefu tena, kwa hiyo akararua nguo zake kwa huzuni,


Lakini Yosefu akawaambia: “Musiogope, mimi ni pahali pa Mungu?


Daudi akapasua nguo yake kwa huzuni. Hata watu waliokuwa pamoja na Daudi wakafanya vilevile.


Halafu Ahabu mufalme wa Israeli akawaita viongozi wote wa inchi, akawaambia: “Sasa, muone jinsi mutu huyu anavyotaka kutuletea hasara! Ametuma ujumbe kwamba anataka wake zangu, watoto wangu, zahabu na feza yangu. Nami sikumukatalia!”


Alipochungulia akamwona mufalme mupya akisimama karibu na nguzo kwenye kiingilio cha hekalu kama ilivyokuwa desturi nao wakubwa wa waaskari na wapiga baragumu wakiwa pembeni ya mufalme, na wakaaji wote wakishangilia na kupiga baragumu. Basi, akapasua nguo zake na kusema kwa sauti kubwa: “Uasi! Uasi!”


Kisha Eliakimu mwana wa Hilkia aliyekuwa musimamizi wa nyumba ya kifalme, Sebuna aliyekuwa katibu, na Yoa mwana wa Asafu mwandishi, wakamwendea Hezekia wakiwa na nguo zenye kupasuliwa, wakamwelezea maneno ya yule jemadari.


Barua yenyewe iliandikwa hivi: “Ninakutumia jemadari wangu Namani pamoja na barua hii, kusudi upate kumuponyesha ugonjwa wake.”


Lakini, ingawa mufalme na watumishi wake wote waliyasikia maneno hayo yote, hawakuogopa wala kurarua nguo zao kwa huzuni.


Jambo unalouliza, ee mufalme, ni gumu. Hakuna mutu anayeweza kukufunulia isipokuwa miungu peke yake ambayo haikai kati ya wanadamu.


Halafu watasema: Tuende tumurudilie Yawe! Yeye mwenyewe ameturarua, lakini yeye mwenyewe atatuponyosha. Yeye mwenyewe ametuumiza, lakini yeye mwenyewe atatunza vidonda.


Yoshua mwana wa Nuni, na Kalebu mwana wa Yefune, ambao walikuwa kati ya wale watu waliokwenda kupeleleza hiyo inchi, wakararua nguo zao


Halafu Kuhani Mukubwa akapasua nguo zake na kusema: “Mutu huyu amemutukana Mungu! Hatuhitaji tena ushuhuda wowote juu yake. Angalia, munatoka kusikia jinsi alivyomutukana Mungu.


wakimupima kusudi wapate kumunasa katika masemi yake.


Lakini Barnaba na Paulo waliposikia habari ile, wakapasua nguo zao kwa huzuni, wakaingia haraka katikati ya kundi la watu, na kusema kwa sauti:


Wangekuwa na hekima wangejua kwa nini walishindwa, wangeweza kuelewa mwisho wao utakuwa namna gani.


Muone kwamba mimi ni Mungu na wala hakuna mwingine isipokuwa mimi. Mimi ninaua na kuweka uzima, ninaumiza na kuponya, na hakuna anayeweza kumwokoa yeyote toka katika mikono yangu.


Yawe anaua na kufufua, yeye anawashusha katika kuzimu naye anawarudisha tena.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ