Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Wafalme 4:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Naye Elisha akamwambia Gehazi: “Umwambie, tumeona jinsi alivyotushugulikia; sasa anataka tumutendee jambo gani? Angependa aombewe lolote kwa mufalme au kwa jemadari wa waaskari?” Mama Musunami akamujibu: “Mimi ninaishi kati ya watu wangu.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Wafalme 4:13
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, sitatwaa kitu chochote isipokuwa tu vile vitu ambayo vijana wangu walikula na sehemu ya wale waliokuwa pamoja nami – Aneri, Eskoli na Mamure – ambao wana haki nayo.”


Ninyi ni wandugu zangu, ninyi ni damu yangu. Kwa nini mukuwe wa mwisho kunirudisha mimi mufalme kwangu?


Mungu atamwazibu Yoabu kwa mauaji hayo aliyoyafanya bila baba yangu kuwa na habari. Yeye aliwaua watu wawili ambao walikuwa wa maana zaidi kuliko yeye, tena walimupita kwa wema; aliwaua Abeneri mwana wa Neri, jemadari wa kundi la waaskari Waisraeli, na Amasa mwana wa Yeteri, jemadari wa waaskari wa Yuda.


Akamwambia mutumishi wake Gehazi: “Umwite yule mama Musunami.” Alipomwita akakuja na kusimama mbele yake.


Elisha akasema: “Tumufanyie nini basi?” Gehazi akamujibu: “Hakika hana mutoto, na mume wake amekuwa muzee.”


Elisha alikuwa amemwambia mwanamuke aliyeishi Sunemu ambaye alikuwa amemufufua mwana wake: “Ondoka na jamaa yako, uhamie katika inchi ya kigeni kwa sababu Yawe ameleta njaa itakayokuwa katika inchi kwa muda wa miaka saba.”


Alipofika, aliwakuta wakubwa wa waaskari katika mukutano. Akasema: “Nina ujumbe wako, mukubwa.” Yehu akamwuliza: “Ni nani kati yetu unayemwambia?” Akamujibu: “Wewe, mukubwa.”


Umutumainie Yawe na kutenda mazuri, upate kuishi katika inchi na kuwa salama.


Mumupokee kwa ajili ya Bwana, kama vile watu wa Mungu wanavyopaswa kufanya. Mumusaidie katika kila jambo atakalohitaji toka kwenu, maana yeye amewasaidia watu wengi na hata mimi peke yangu vilevile.


Munisalimie Maria, aliyewashugulikia sana.


Musijiachilie kutawaliwa na tamaa ya mali katika maisha yenu, lakini mutoshelewe na vitu munavyokuwa navyo, kwa maana Mungu mwenyewe amesema: “Sitakusahau wala kukuachilia.”


Kwa maana Mungu ni mwenye haki. Yeye hatasahau kazi yenu na upendo mulioonyesha kwa ajili yake kwa namna mulivyowasaidia watu wake na munavyoendelea kuwasaidia.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ