Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Wafalme 4:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Basi, mwanamuke mumoja kati ya wake za wanafunzi wa manabii akamwendea Elisha, akamwambia: “Mutumishi wako, mume wangu amekufa, na kama vile unavyojua, alikuwa mwenye kumwogopa Mungu. Lakini mutu aliyemukopesha feza amekuja kuwatwaa wana wangu wawili wakuwe watumwa wake.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Wafalme 4:1
35 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Malaika akamwambia: “Usinyooshe mukono wako juu ya kijana wala usimufanyie jambo lolote! Sasa ninajua kwamba unamwogopa Mungu, maana haukuninyima hata mwana wako wa pekee.”


Basi, Ahabu akamwita Obadia musimamizi wa nyumba ya kifalme. Obadia alikuwa mutu anayemwogopa Yawe sana,


Kwa amri ya Yawe, mumoja wa wanafunzi wa manabii akamwambia mwenzake: “Unipige, tafazali.” Lakini mwenzake akakataa kumupiga.


Wale wanafunzi wa manabii kutoka Yeriko walipomwona, walisema: “Roho wa Elia yuko kwa Elisha.” Basi, wakaenda kumupokea, wakainama mbele yake kwa heshima.


Wanafunzi wa manabii wa Beteli wakamwendea Elisha, wakamwuliza: “Unajua kwamba leo Yawe atamupeleka bwana wako?” Elisha akajibu: “Ndiyo. Ninajua. Munyamaze.”


Wanafunzi wa manabii wa Yeriko wakamwendea Elisha, wakamwuliza: “Unajua kwamba leo Yawe atamupeleka bwana wako?” Elisha akawajibu: “Ndiyo. Ninajua. Munyamaze.”


Manabii makumi tano wakawafuata mpaka kwenye muto Yordani. Elia na Elisha wakasimama karibu na muto, nao manabii wakasimama mbali kidogo.


Elisha akarudi Gilgali wakati katika inchi kulikuwa njaa. Siku moja, alipokuwa akifundisha wanafunzi wa manabii alimwambia mutumishi wake: “Weka chungu kikubwa juu ya moto, uwapikie manabii chakula.”


Lakini Elisha akamupelekea mufalme wa Israeli habari afanye angalisho na pahali pale, kwa sababu Waaramu walikuwa tayari kupashambulia.


Wabinti zetu hatutawaoesha kwa watu wa inchi hii na wala wana wetu hawataoa kwao.


nikamuchagua ndugu yangu Hanani kuwa mwangalizi wa Yerusalema akishirikiana na Hanania aliyekuwa jemadari wa waaskari walinzi wa munara katika Yerusalema; kwa sababu alikuwa mutu wa kutegemewa na anayemwogopa sana Mungu, hapakukuwa mwingine aliyelingana naye,


Kama vile anga linavyokuwa juu mbali na dunia, ndivyo kipimo cha wema wake kinavyokuwa kwa watu wanaomwabudu.


Lakini wema wa Yawe unadumu milele, kwa wale wote wanaomwabudu; na haki yake inadumu vizazi vyote,


atawabariki wote wanaomwabudu, atawabariki wakubwa kama vile wadogo.


lakini anapendezwa na watu wanaomuheshimu, ndio wanaotegemea wema wake.


Tajiri anamutawala masikini. Mwenye kukopesha ni mutumwa wa mwenye kukopeshwa.


Nyuma ya hayo yote yaliyokwisha kusemwa, kungali hili linalotakiwa: Umwogope Mungu, na ushike amri zake, kwa sababu hayo ndiyo mapaswa ya mwanadamu.


Wenye zambi wanatenda maovu mara mia. Hata hivyo, wanaendelea kuishi. Lakini, mimi ninajua kwamba itakuwa heri kwa wanaomwogopa Mungu, kwa sababu ya woga wao.


Yawe anasema hivi: Kama nimeachana na mama yako Yerusalema, barua ya kuachana iko wapi? Nilikuwa na deni ya nani kwa kuwauzisha? Mukumbuke kwamba muliuzishwa kwa ajili ya maovu yenu, mama yenu alifukuzwa kwa ajili ya makosa yenu.


Kila mwaka wa saba, kila mumoja wenu atamwachilia huru ndugu yake Muyuda aliyeuzishwa kuwa mutumwa kwa muda wa miaka sita. Munapaswa kuwaachilia huru, wasiwatumikie tena. Lakini babu zenu hawakunisikiliza wala kunitegea sikio.


anaweza kukombolewa kisha kujiuzisha, mumoja wa wandugu zake anaweza kumukomboa.


Halafu watu wanaomutii Yawe walizungumuza wao kwa wao, naye Yawe akasikia mazungumuzo yao. Mbele yake kukawekwa kitabu ambamo uliandikwa ukumbusho wa wale wanaomutii na kumuheshimu.


Na kwa kuona mutumishi yule hakukuwa na jinsi ya kulipa deni lile, bwana wake akaamuru auzishwe kuwa mutumwa, yeye na muke wake pamoja na watoto wake na vyote alivyokuwa navyo viuzishwe vilevile, kusudi apate kumulipa.


Lakini hakutaka, akamupeleka katika kifungo mpaka atakapolipa deni lile.


Yesu akaongeza kusema: “Ni hivi vilevile Baba yangu anayekuwa mbinguni atakavyowatendea ninyi, kama kila mumoja wenu asipomusamehe ndugu yake kwa moyo wake wote.”


“Wandugu zangu, ninyi wazao wa Abrahamu na ninyi watu wa mataifa mengine munaokuwa hapa kwa kumwabudu Mungu, habari hii ya wokovu imetumwa kwetu!


Kwa sababu Mungu hatahurumia mutu yule asiyehurumia wengine. Lakini huruma ya Mungu itaishinda hukumu.


Ewe Bwana, hakuna asiyekuogopa, wala hakuna asiyekutukuza, kwa maana wewe peke yako ndiwe mutakatifu. Mataifa yote yatakuja kukuabudu, kwa maana matendo yako ya haki yameonyeshwa wazi.”


Kisha sauti ikasikilika toka kwenye kiti cha kifalme ikasema: “Mumusifu Mungu wetu ninyi watumishi wake wote, ninyi wote munaomuheshimu, wakubwa na wadogo!”


Lakini Elimeleki, mume wa Naomi, akakufa na Naomi akaachwa na wana wake.


Watu wote waliogandamizwa au waliokuwa na madeni au wale wenye huzuni walijiunga na Daudi. Jumla yao ilikuwa watu yapata mia ine, naye akakuwa kiongozi wao.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ