Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Wafalme 3:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Hata hivyo, Yoramu aliendelea kutenda zambi ileile ya Yeroboamu mwana wa Nebati ambaye aliwasukuma watu wa Israeli watende zambi. Hakuiacha.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Wafalme 3:3
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yeroboamu hakuuacha upotovu wake; aliendelea kuchagua watu wa kawaida kuwa makuhani, watumike kwa nafasi ya kutambikia juu ya vilima. Mutu yeyote aliyejitolea, alimutakasa kuwa kuhani wa nafasi ya kutambikia kule juu ya vilima.


Yawe ataitupilia Israeli kwa sababu ya zambi za Yeroboamu ambaye alitenda zambi na kuwasukuma watu wa Israeli vilevile watende zambi.”


Wewe umetenda uovu mubaya zaidi kuliko waliotenda wale waliokutangulia. Wewe umenikasirikisha kwa kujitengenezea miungu mingine na sanamu za kufua, kisha umeniacha.


Nadabu alitenda maovu mbele ya Yawe; alifuata mwenendo wa baba yake na kutenda zambi ileile ambayo aliwasukuma watu wa Israeli watende.


Basha alitenda maovu mbele ya Yawe; alifuata mwenendo wa Yeroboamu na kutenda zambi ileile ambayo aliwasukuma watu wa Israeli watende.


Tena, zaidi ya kufuata mwenendo mubaya wa Yeroboamu mwana wa Nebati, Ahabu alimwoa Yezebeli binti ya Etibali mufalme wa Wasidoni. Akamutumikia na kumwabudu Bali.


Yoasi vilevile alitenda maovu mbele ya Yawe. Hakuacha zambi zile za Yeroboamu mwana wa Nebati ambaye aliwasukuma watu wa Israeli watende zambi. Aliendelea kuzitenda.


Alitenda maovu mbele ya Yawe. Alitenda zambi sawa na Yeroboamu mwana wa Nebati ambaye aliwasukuma watu wa Israeli watende zambi. Hakuacha kutenda zambi hii.


Hata hivyo hawakuacha zambi za mufalme Yeroboamu ambaye aliwasukuma watu wa Israeli watende zambi; lakini waliendelea na zambi zao na sanamu ya Ashera ilibakia kule Samaria.


Alitenda maovu mbele ya Yawe; hakuacha zile zambi zote za Yeroboamu mwana wa Nebati ambaye aliwasukuma watu wa Israeli watende zambi.


Alitenda maovu mbele ya Yawe. Hakuacha maovu ya Yeroboamu mwana wa Nebati, ambaye aliwasukuma watu wa Israeli watende zambi.


Naye, kama vile watangulizi wake, alitenda maovu mbele ya Yawe; hakuacha zambi zile za Yeroboamu mwana wa Nebati ambaye aliwasukuma watu wa Israeli watende zambi.


Nyuma ya Yawe kutenga Israeli kutoka ukoo wa Daudi walimuweka Yeroboamu mwana wa Nebati kuwa mufalme. Naye Yeroboamu aliwasukuma watu wa Israeli kumwacha Yawe na kutenda zambi kubwa sana.


Waisraeli walitenda zambi zote Yeroboamu alizotenda. Hawakuziacha


mpaka kwa mwisho Yawe akawafukuza kutoka mbele yake, kama vile alivyokuwa amesema kupitia kwa watumishi wake wote manabii. Kwa hiyo watu wa Israeli walipelekwa katika uhamisho kutoka katika inchi yao wenyewe mpaka Asuria ambako wanakaa hata sasa.


Zaidi ya mambo hayo, Manase aliwaangusha watu wa Yuda katika zambi kwa kutenda maovu mbele ya Yawe. Aliwaua watu wengi wasiokuwa na kosa, damu ikajaa toka upande mumoja mpaka upande mwingine wa Yerusalema.


Zaidi ya hayo aliharibu kule Beteli pahali pa kuabudia palipojengwa na mufalme Yeroboamu mwana wa Nebati ambaye aliwasukuma watu wa Israeli watende zambi. Aliharibu mazabahu hayo na kuvunja mawe yake vipandevipande, na kisha akaviponda mpaka vikakuwa mavumbi. Vilevile akachoma sanamu ya Ashera.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ