Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Wafalme 24:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Hakika mambo haya yakaitokea inchi ya Yuda kwa amri ya Yawe, kwa kuwahamisha kutoka mbele yake, kwa sababu ya zambi za mufalme Manase na yote aliyoyatenda,

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Wafalme 24:3
27 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ninyi mulitaka kunitendea vibaya, lakini Mungu alikusudia mema kusudi watu wengi wapate kuwa wazima kama vile munavyoona leo.


Basi, Yawe akawakasirikia sana watu wa Israeli na kuwafukuza kabisa mbele yake; hakuacha mutu isipokuwa kabila la Yuda peke yake.


Yawe aliwakataa Waisraeli wote; akawaazibu na kuwaacha katika mikono ya waadui wakali, na kisha akawafukuza mbele yake.


mpaka kwa mwisho Yawe akawafukuza kutoka mbele yake, kama vile alivyokuwa amesema kupitia kwa watumishi wake wote manabii. Kwa hiyo watu wa Israeli walipelekwa katika uhamisho kutoka katika inchi yao wenyewe mpaka Asuria ambako wanakaa hata sasa.


Zaidi ya hayo, munafikiri nimekuja bila amri ya Yawe kwa kuishambulia na kuiangamiza inchi hii? Yawe ndiye aliyeniambia: Uishambulie inchi hii na kuiangamiza!”


Zaidi ya mambo hayo, Manase aliwaangusha watu wa Yuda katika zambi kwa kutenda maovu mbele ya Yawe. Aliwaua watu wengi wasiokuwa na kosa, damu ikajaa toka upande mumoja mpaka upande mwingine wa Yerusalema.


Yawe aliwakasirikia sana watu wa Yerusalema na Yuda, hata akawafukuza mbali naye. Zedekia alimwasi mufalme wa Babeli.


Ingawa jeshi la Suria lilikuwa dogo, Yawe alilipatia ushindi mbele ya jeshi kubwa la watu wa Yuda kwa sababu hao watu wa Yuda walikuwa wamemwacha Yawe, Mungu wa babu zao. Hivi, Wasuria wakatimiza azabu ya Mungu juu ya mufalme Yoasi.


Na alipokuwa angali akisema naye, Amazia akamwambia: “Nyamaza! Tulikufanya wewe kuwa mushauri wa mufalme? Kwa nini uawe?” Nabii akanyamaza, lakini akasema: “Ninafahamu kwamba Mungu ameamua kukuangamiza kwa maana umetenda haya yote, kisha unazarau shauri langu.”


Usiiname mbele yao wala kuvitumikia, kwa sababu mimi Yawe, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu. Ninawaazibu wana kwa ajili ya maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha ine cha wale wanaonichukia.


Mimi ninafanya mwangaza na kuumba giza; ninaleta uheri na kusababisha hasara. Mimi Yawe ninatenda vitu hivi vyote.


Muji huu umechochea hasira yangu na kuniuzi tangu siku ulipojengwa mpaka leo hii. Kwa hiyo, nitauondoa kabisa mbele yangu,


Hii ndiyo hesabu ya watu ambao Nebukadneza aliowapeleka katika uhamisho kwa mwaka wa saba wa utawala wake: Wayuda elfu tatu na makumi mbili na watatu.


Uuambie kwamba: Bwana wetu Yawe anasema hivi: Wewe ni muji unaowaua watu wako mwenyewe na kujichafua kwa kufanya sanamu za miungu; kwa hiyo wakati wako wa azabu umetimia.


Basi, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Ole kwake muji wa mauaji! Muji huo ni kama chungu chenye kutu, ambacho kutu yake haiwezi kutoka! Vipande vya nyama ndani yake vinatoshwa kimoja kimoja bila kuchaguliwa.


Baragumu ya vita inalia katika muji bila kutia watu hofu? Muji unaweza kupatwa na hasara ambayo haikuletwa na Mungu?


Musimame! Muende! Hapa hakuna tena pahali pa kupumzika! Kwa ajili ya ukosefu wenu wa uaminifu, maangamizi makubwa yanawangojea!


Kama vile Yawe alivyopendezwa kuwafanikisha na kuwafanya kuwa wengi, ni vile vile Yawe atapendezwa kuwaletea hasara na kuwaangamiza. Nanyi mutaondolewa katika inchi hiyo ambayo munakwenda kuirizi.


“Mambo ya siri ni ya Yawe, Mungu wetu, lakini yale ambayo ameyafunua ni yetu na wazao wetu milele, kusudi tushike maneno yote ya sheria hii.”


Lakini kama vile Yawe, Mungu wenu, alivyotimiza mambo yote mema aliyowaahidi, ni vile vile anavyoweza kuwaletea maovu yote mpaka awaangamize wote kutoka inchi hii nzuri ambayo amewapa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ