Kisha, mufalme Hiramu wa Tiro alituma wajumbe kwa Daudi. Alimupelekea vilevile miti ya mierezi, waseremala na wajengaji ambao walimujengea Daudi nyumba ya kifalme.
Halafu kisha kuzipima walizitoa kwa wafanyakazi waliosimamia nyumba ya Yawe, nao wakazilipa kwa waseremala na wenye kujenga waliotengeneza nyumba ya Yawe,
Daudi akatoa amri kwamba wageni wote waliokuwa katika inchi ya Israeli wakusanyike, naye akawapangia kazi. Akaweka wamoja wachonge vizuri mawe ya kujenga nyumba ya Mungu.