Yoasi akaita makuhani na kuwaamuru, akisema: “Kila kuhani apokee feza yote inayotolewa katika nyumba ya Yawe: ni kusema malipo ya kodi za hekalu na matoleo ya mapenzi. Azipokee kutoka kwa yeyote anayemufahamu kwa kutengeneza nyumba popote panapohitajika.”
Walipomwita mufalme Hezekia walipokelewa na Eliakimu mwana wa Hilkia ambaye alikuwa musimamizi wa nyumba ya kifalme, Sebuna aliyekuwa mwandishi wa mufalme, na Yoa mwana wa Asafu, mwandishi wa habari.
Salumu mwana wa Kore mwana wa Ebiasafu, pamoja na wandugu zake wa ukoo wa Kora, walikuwa na kazi ya kutunza viingilio vya hema la mukutano, kama vile babu zake walivyokuwa wakati wa ulinzi wa kambi ya Yawe.
Akifuata maagizo ya Daudi baba yake, alipanga zamu za kila siku za makuhani na za Walawi waliowasaidia makuhani kusifu na kutimiza kazi zao. Vilevile aliwapanga walinzi wa milango katika makundi aliyoweka kwa kulinda kila mulango; maana ndivyo Daudi, mutu wa Mungu alivyoamuru.
Walinzi wa milango waliokaa katika Yerusalema walikuwa: Akubu na Talmoni pamoja na wandugu zao waliokuwa wakilinda milango, walikuwa mia moja makumi saba na wawili.