2 Wafalme 22:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
3 Katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wake, mufalme alimutuma Safanu mwana wa Azalia, mujukuu wa Mesulamu, mwandishi katika nyumba ya Yawe akisema:
Yehoyada akatwaa sanduku na kutoboa tundu kwenye kifuniko chake, kisha akaliweka kwenye mazabahu upande wa kuume, mutu anapoingia katika nyumba ya Yawe. Nao makuhani waliokuwa wakichunga kwenye mulango waliweka ndani ya sanduku feza zote zilizotolewa katika nyumba ya Yawe.
Basi, Baruku alisoma maneno ya Yeremia kutoka katika kile kitabu mbele ya watu wote, ndani ya nyumba ya Yawe, katika chumba cha Gemaria mwana wa Safanu aliyekuwa katibu. Chumba hicho kilikuwa katika baraza la juu, kwenye mulango mupya wa nyumba ya Yawe.
alikwenda kwenye nyumba ya kifalme na kuingia katika chumba cha katibu. Mule mulikuwa wakubwa wote: katibu Elisama, Delaya mwana wa Semaya, Elnatana mwana wa Akibori, Gemaria mwana wa Safanu, Zedekia mwana wa Hanania, na wakubwa wote.