Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Wafalme 22:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wake, mufalme alimutuma Safanu mwana wa Azalia, mujukuu wa Mesulamu, mwandishi katika nyumba ya Yawe akisema:

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Wafalme 22:3
7 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yehoyada akatwaa sanduku na kutoboa tundu kwenye kifuniko chake, kisha akaliweka kwenye mazabahu upande wa kuume, mutu anapoingia katika nyumba ya Yawe. Nao makuhani waliokuwa wakichunga kwenye mulango waliweka ndani ya sanduku feza zote zilizotolewa katika nyumba ya Yawe.


Lakini, katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Yosia, Pasaka ilisherehekewa kwa Yawe katika Yerusalema.


Neno la Yawe lilimufikia Yeremia katika mwaka wa kumi na tatu wa utawala wa Yosia mwana wa Amoni, mufalme wa Yuda.


Basi, Baruku alisoma maneno ya Yeremia kutoka katika kile kitabu mbele ya watu wote, ndani ya nyumba ya Yawe, katika chumba cha Gemaria mwana wa Safanu aliyekuwa katibu. Chumba hicho kilikuwa katika baraza la juu, kwenye mulango mupya wa nyumba ya Yawe.


Mikaya mwana wa Gemaria, mujukuu wa Safanu, aliposikia maneno yote ya Yawe ambayo yalisomwa kutoka kile kitabu,


alikwenda kwenye nyumba ya kifalme na kuingia katika chumba cha katibu. Mule mulikuwa wakubwa wote: katibu Elisama, Delaya mwana wa Semaya, Elnatana mwana wa Akibori, Gemaria mwana wa Safanu, Zedekia mwana wa Hanania, na wakubwa wote.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ