Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Wafalme 22:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Yosia alitenda kwa usawa mbele ya Yawe. Alifuata mienendo yote ya babu yake Daudi; hakuiacha hata kidogo.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Wafalme 22:2
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Na kama utashika yote nitakayokuamuru, kama utaishi kulingana na mapenzi yangu, kama utatenda mema mbele yangu kwa kushika masharti yangu na amri zangu, kama vile mutumishi wangu Daudi alivyofanya, mimi nitakuwa pamoja nawe siku zote. Na nitakupatia inchi ya Israeli na kuufanya utawala wako ukuwe imara kama nilivyomufanyia Daudi.


Mufalme Asa alitenda mambo yanayokuwa mema mbele ya Yawe kama vile Daudi babu yake alivyofanya.


Yawe alifanya hivyo kwa sababu Daudi alitenda mema mbele yake na hakuenda pembeni ya maagizo ya Yawe siku za maisha yake yote, isipokuwa tu lile jambo la Uria Muhiti.


Solomono akamwambia: “Ulimwonyesha wema mwingi mutumishi wako Daudi, baba yangu, kwa sababu alikutumikia kwa uaminifu, kwa haki na kwa moyo wa usawa; na umedumisha mema yako kwa kumupa mwana anayeikaa sasa kwenye kiti chake cha kifalme.


Wakati wa maisha yake yote alitenda kwa usawa mbele ya Yawe, kwa sababu kuhani Yehoyada alikuwa akimufundisha.


Alitenda kwa usawa mbele ya Yawe, lakini hakukuwa kama babu yake Daudi. Akafanya mambo yote kama vile baba yake Yoasi.


Alikuwa na umri wa miaka makumi mbili alipoanza kutawala. Akatawala kwa muda wa miaka kumi na sita akiwa kule Yerusalema. Hakutenda kwa usawa mbele ya Yawe kama vile Daudi babu yake alivyofanya,


Alitenda kwa usawa mbele ya Yawe, kama vile Daudi babu yake alivyotenda.


Yawe alikuwa pamoja na Yosafati kwa sababu alifuata njia za kwanza za babu yake Daudi, wala hakumwabudu mungu Bali.


Alitenda kwa usawa mbele ya Yawe, kama vile babu yake Daudi alivyotenda.


Hivi ndivyo mufalme Hezekia alivyotenda mambo mema, ya haki na ya uaminifu mbele ya Yawe, Mungu wake, katika inchi yote ya Yuda.


Yosia alikuwa na umri wa miaka minane alipoanza kutawala, alitawala miaka makumi tatu na mumoja akiwa kule Yerusalema.


Hata mutoto anajulikana kwa matendo yake, kama ni safi na sawa.


Usigeukie kuume wala kushoto; epusha muguu wako mbali na uovu.


Hili ni neno la Yawe lililomufikia Zefania mwana wa Kusi, mujukuu wa Gedalia mwana wa Amaria, wa uzao wa mufalme Hezekia, wakati wa utawala wa mufalme Yosia mwana wa Amoni, mufalme wa Yuda:


“Ninyi mukuwe waangalifu mufanye kama vile Yawe alivyowaamuru. Mutimize kila kitu sawasawa.


Ukuwe tu imara na hodari. Ukuwe mwangalifu na kushika sheria yote mutumishi wangu Musa aliyokuamuru. Fuata kila sehemu ya sheria hiyo nawe utafanikiwa popote utakapoenda.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ