Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Wafalme 22:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Yosia alikuwa na umri wa miaka minane alipoanza kutawala akiwa kule Yerusalema na utawala wake ulidumu kwa miaka makumi tatu na mumoja. Mama yake aliitwa Yedida, binti wa Adaya mukaaji wa muji wa Bozikati.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Wafalme 22:1
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mutu huyo akailaani ile mazabahu akisema: “Ee mazabahu, Yawe anasema hivi: ‘Kutazaliwa mutoto katika ukoo wa Daudi, jina lake Yosia. Huyo atawatwaa makuhani wanaotumika kwa nafasi ya ibada na kufukiza ubani juu yako, na kuwatambika juu yako. Hakika, mifupa ya watu itateketezwa juu yako!’ ”


Manase alikuwa na umri wa miaka kumi na miwili alipoanza kutawala Yuda, akatawala kutoka Yerusalema kwa muda wa miaka makumi tano na mitano.


Lakini watu wa Yuda wakawaua wote waliomwua Amoni. Kisha watu hao wa Yuda wakamuweka mwana wake Yosia kuwa mufalme kwa pahali pake.


Amoni akazikwa katika kaburi katika bustani ya Uza. Yosia mwana wake akatawala kwa pahali pake.


Ee Yawe, Bwana wetu, jina lako linatukuzwa sana katika dunia yote! Utukufu wako unaenea mpaka juu ya mbingu!


Ole wako, ewe inchi, mutawala wako akiwa kijana, na viongozi wako wakifanya karamu asubui.


Mungu anasema: Nitaweka watoto kuwa wakubwa wao; watoto wachanga watawatawala.


Neno la Yawe lilimufikia Yeremia katika mwaka wa kumi na tatu wa utawala wa Yosia mwana wa Amoni, mufalme wa Yuda.


Lakini kama mutu yule akiwa na mutoto ambaye ameona zambi ambazo baba yake alitenda, lakini yeye hatendi mabaya yale, hatakufa juu ya uovu wa baba yake. Ni mutoto anayetenda hivi: hakuli sadaka kwenye milima, haziangalii sanamu za miungu ya Waisraeli, hamuchafui muke wa jirani yake, hamutendei mutu yeyote ubaya, hakamati rehani, haibi, anawapatia wenye njaa chakula na kuwavalisha wale wanaokuwa uchi, anaepuka kutenda uovu, anakopesha bila kudai faida wala kujipatia mazidio, anatii maagizo yangu na kufuata masharti yangu.


Hili ni neno la Yawe lililomufikia Zefania mwana wa Kusi, mujukuu wa Gedalia mwana wa Amaria, wa uzao wa mufalme Hezekia, wakati wa utawala wa mufalme Yosia mwana wa Amoni, mufalme wa Yuda:


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ