Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Wafalme 21:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Katika viwanja viwili vya nyumba ya Yawe, alijenga mazabahu ya kuabudia jeshi la mbingu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Wafalme 21:5
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Alijenga uwanja wa ndani ambao kuta zake zilikuwa za mistari tatu ya mawe yaliyochongwa, na mustari moja wa boriti za mwerezi.


Kiwanja cha nyumba ya mufalme kilikuwa na kuta zenye mustari moja wa mbao za mierezi na mistari mitatu ya mawe ya kuchongwa kila moja; ndivyo ilivyokuwa hata kwa kiwanja cha ndani cha nyumba ya Yawe na kwa baraza la nyumba.


Mazabahu ambayo wafalme wa Yuda walijenga juu ya paa kwenye chumba cha juu cha Ahazi, pamoja na mazabahu ambayo Manase alijenga katika viwanja viwili vya nyumba ya Yawe, aliyabomoa na kuyapondaponda, kisha alitupa mavumbi yake katika kijito cha Kidroni.


Kisha Yosia akaamuru Kuhani Mukubwa Hilkia na makuhani wasaidizi wake na walinzi wa mulango watoe katika hekalu la Yawe vitu vilivyotengenezwa kwa ajili ya Bali, Ashera na kwa ajili ya jeshi la mbingu. Aliviteketeza inje ya Yerusalema katika bonde la Kidroni na kupeleka majivu yake kule Beteli.


Kisha akawaondoa makuhani wote waliobarikiwa na wafalme wa Yuda kwa kufukiza ubani katika pahali pa kuabudia katika miji ya Yuda na kunzunguka Yerusalema, vilevile wale waliofukiza ubani kwa Bali, jua, mwezi, nyota na jeshi la mbingu katika nyumba ya Yawe.


Naye aliondoa sanamu ya Ashera kutoka katika nyumba ya Yawe, inje ya Yerusalema, akaipeleka mpaka kwenye kijito cha Kidroni. Kule akaiteketeza na kuisaga mpaka ikakuwa mavumbi, nayo mavumbi yake akayatawanya juu ya makaburi ya watu.


Akatoa katika nyumba ya Yawe miungu yote ya kigeni na sanamu pamoja na mazabahu zote alizokuwa amejenga kwenye mulima wa nyumba ya Yawe na katika Yerusalema; akavitupa inje ya muji.


Alijenga mazabahu za kuabudia jeshi la mbinguni kwenye viwanja vya nyumba ya Yawe.


Akatengeneza kiwanja cha ndani cha makuhani na kingine kikubwa cha inje, na milango ya kiwanja ambayo aliifunika na shaba;


Yule mutu akanipitisha kwenye njia ya kuingilia upande wa kusini, tukafika kwenye kiwanja cha ndani. Aliipima hiyo njia nayo ilikuwa sawa na zile njia zingine za kuingilia kwenye kuta za inje.


Yule mutu alinipeleka upande wa mashariki wa kiwanja cha ndani. Akaipima ile njia ya kuingilia, nayo ilikuwa na urefu kama zile njia zingine za kuingilia.


Ile baraza ya kuingilia ilikuwa inaelekea kwenye kiwanja cha inje; kulikuwa miti ya ngazi iliyochorwa kwenye kuta za hiyo nafasi ya kupitia. Kulikuwa vilevile ngazi nane za kupandia kuelekea kwenye mulango huu.


Yule mutu akapima kiwanja cha ndani, nacho kilikuwa muraba: pande zote zilikuwa na upana wa metre makumi tano. Mazabahu yalikuwa mbele ya nyumba ya Yawe.


Kulikuwa gorofi tatu zilizounganisha metre kumi za kiwanja cha ndani na zikielekea sakafu ya kiwanja cha inje.


Kisha roho akanitwaa na kunipeleka kwenye kiwanja cha ndani. Nikaona utukufu wa Yawe ukiwa umeijaza nyumba ya Yawe.


Watakapotoka kwenda kwenye kiwanja cha inje kwa watu, watatosha nguo walizovaa wakati walipokuwa wanatumika na kuziweka katika vyumba vitakatifu. Ni lazima wavae nguo zingine, kusudi watu wasijitakase kwa kugusa nguo zao.


Kisha akanipeleka mpaka katika uwanja wa ndani wa nyumba ya Yawe. Huko kwenye mulango wa hekalu, kati ya baraza na mazabahu, kulikuwa wanaume yapata makumi mbili na watano, wakigeuzia mugongo wao upande wa hekalu, na nyuso zao zikielekea upande wa mashariki. Walikuwa wanaabudu jua wakielekea upande wa mashariki.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ