Lakini baba yake akakataa, akisema: “Ninajua, mwana wangu, ninajua. Wana wa Manase vilevile watakuwa taifa na wakubwa. Hata hivyo, ndugu yake mudogo atakuwa mukubwa kuliko yeye na wazao wake watakuwa mataifa mengi.”
Wanafunzi wa manabii wa Beteli wakamwendea Elisha, wakamwuliza: “Unajua kwamba leo Yawe atamupeleka bwana wako?” Elisha akajibu: “Ndiyo. Ninajua. Munyamaze.”
Basi, mwanamuke mumoja kati ya wake za wanafunzi wa manabii akamwendea Elisha, akamwambia: “Mutumishi wako, mume wangu amekufa, na kama vile unavyojua, alikuwa mwenye kumwogopa Mungu. Lakini mutu aliyemukopesha feza amekuja kuwatwaa wana wangu wawili wakuwe watumwa wake.”
Gehazi akajibu: “Mambo yote ni sawa lakini tu bwana wangu amenituma nikuambie kwamba sasa hivi amepokea watu wawili wa kundi la manabii katika inchi ya milima ya Efuraimu, naye angependa uwape vikoroti elfu tatu vya feza na nguo mbili ya sikukuu.”
Wakati uleule nabii Elisha alimwita mumoja wa wanafunzi wa nabii, akamwambia: “Ujitayarishe kusafiri, twaa chupa hii ya mafuta, na kwenda Ramoti katika Gileadi.
Mungu anasema hivi: Enyi wakaaji wa mbali munyamaze munisikilize! Enyi mataifa mujitie moyo; mujitokeze na mujisemee, na mukuje tuende pamoja kwa hukumu.
Watu hao wakawaambia: “Ninyi Wagalilaya, sababu gani munasimama pale mukiangalia mbinguni? Huyu Yesu aliyenyanyuliwa toka katikati yenu kwenda mbinguni, atarudi sawa vile mulivyomwona akienda.”
mpaka siku ile aliponyanyuliwa mbinguni. Mbele ya kunyanyuliwa kule, alitoa maagizo kwa njia ya Roho Mutakatifu kwa watu aliokuwa amewachagua kuwa mitume wake.
Kisha, utafika kule Gibeati-Elohimu, pahali ambapo pana kambi ya waaskari wa Wafilistini. Pale, utakapokuwa unakaribia muji, utakutana na kundi la manabii. Manabii hao watakuwa wanatoka kwenye nafasi ya kuabudia na wakipiga vinubi, matari, filimbi na zeze, na watakuwa wanatabiri.