Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Wafalme 2:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Wanafunzi wa manabii wa Yeriko wakamwendea Elisha, wakamwuliza: “Unajua kwamba leo Yawe atamupeleka bwana wako?” Elisha akawajibu: “Ndiyo. Ninajua. Munyamaze.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Wafalme 2:5
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini baba yake akakataa, akisema: “Ninajua, mwana wangu, ninajua. Wana wa Manase vilevile watakuwa taifa na wakubwa. Hata hivyo, ndugu yake mudogo atakuwa mukubwa kuliko yeye na wazao wake watakuwa mataifa mengi.”


Kwa amri ya Yawe, mumoja wa wanafunzi wa manabii akamwambia mwenzake: “Unipige, tafazali.” Lakini mwenzake akakataa kumupiga.


Wanafunzi wa manabii wa Beteli wakamwendea Elisha, wakamwuliza: “Unajua kwamba leo Yawe atamupeleka bwana wako?” Elisha akajibu: “Ndiyo. Ninajua. Munyamaze.”


Basi, mwanamuke mumoja kati ya wake za wanafunzi wa manabii akamwendea Elisha, akamwambia: “Mutumishi wako, mume wangu amekufa, na kama vile unavyojua, alikuwa mwenye kumwogopa Mungu. Lakini mutu aliyemukopesha feza amekuja kuwatwaa wana wangu wawili wakuwe watumwa wake.”


Gehazi akajibu: “Mambo yote ni sawa lakini tu bwana wangu amenituma nikuambie kwamba sasa hivi amepokea watu wawili wa kundi la manabii katika inchi ya milima ya Efuraimu, naye angependa uwape vikoroti elfu tatu vya feza na nguo mbili ya sikukuu.”


Siku moja, wanafunzi wa manabii walimulalamikia Elisha wakisema: “Pahali hapa tunapokaa ni padogo sana kwetu!


Wakati uleule nabii Elisha alimwita mumoja wa wanafunzi wa nabii, akamwambia: “Ujitayarishe kusafiri, twaa chupa hii ya mafuta, na kwenda Ramoti katika Gileadi.


wakati wa kupasua na wakati wa kushona, wakati wa kukaa kimya na wakati wa kusema,


Mungu anasema hivi: Enyi wakaaji wa mbali munyamaze munisikilize! Enyi mataifa mujitie moyo; mujitokeze na mujisemee, na mukuje tuende pamoja kwa hukumu.


Amosi akamujibu Amazia: Mimi si nabii wa mushahara, wala si mumoja wa kikundi cha manabii. Mimi ni muchungaji na mulimaji wa miti ya mikuyu.


Lakini Yawe yuko katika hekalu lake takatifu; dunia yote ikae kimya mbele yake.


Alipokuwa akiwabariki akajitenga nao na kunyanyuliwa mbinguni.


Watu hao wakawaambia: “Ninyi Wagalilaya, sababu gani munasimama pale mukiangalia mbinguni? Huyu Yesu aliyenyanyuliwa toka katikati yenu kwenda mbinguni, atarudi sawa vile mulivyomwona akienda.”


mpaka siku ile aliponyanyuliwa mbinguni. Mbele ya kunyanyuliwa kule, alitoa maagizo kwa njia ya Roho Mutakatifu kwa watu aliokuwa amewachagua kuwa mitume wake.


Paulo akamujibu: “Muheshimiwa Festo, mimi si mwenda-wazimu. Maneno ninayosema ni ya kweli nayo ni ya maana.


Kisha, utafika kule Gibeati-Elohimu, pahali ambapo pana kambi ya waaskari wa Wafilistini. Pale, utakapokuwa unakaribia muji, utakutana na kundi la manabii. Manabii hao watakuwa wanatoka kwenye nafasi ya kuabudia na wakipiga vinubi, matari, filimbi na zeze, na watakuwa wanatabiri.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ