Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Wafalme 2:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Kisha Elia akamwambia Elisha: “Tafazali ubakie hapa. Yawe amenituma niende Yeriko.” Lakini Elisha akakataa akisema: “Kama vile Yawe anavyoishi na kama vile unavyoishi, sitakuacha.” Basi, wakaenda pamoja mpaka Yeriko.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Wafalme 2:4
10 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wakati wa utawala wake, Hieli wa muji wa Beteli aliujenga upya muji wa Yeriko. Na sawa kabisa na neno Yawe alilosema kwa njia ya Yoshua mwana wa Nuni, Hieli alikufiwa na muzaliwa wake wa kwanza aliyeitwa Abiramu, wakati wa kuiweka misingi ya Yeriko. Akakufiwa vilevile na mwana wake mudogo aliyeitwa Segubu, wakati wa kuweka milango ya muji wa Yeriko.


Walipokuwa katika njia, Elia akamwambia Elisha: “Tafazali ubakie hapa. Yawe amenituma niende Beteli.” Lakini Elisha akamwambia: “Kama vile Yawe anavyoishi na kama vile unavyoishi, sitakuacha.” Basi, wakaenda pamoja mpaka Beteli.


Mwanamuke akamwambia Elisha: “Kama vile Yawe anavyoishi na kama vile unavyoishi, sitakuacha.” Basi Elisha akaondoka na kufuatana naye.


Yesu alipoingia katika muji Yeriko, akapita katikati yake.


Naye alipofika, akaona mambo yote yaliyotendeka kutokana na neema ya Mungu, akafurahi, naye akawatia wanafunzi wote moyo kusudi waendelee kushikamana na Bwana kwa moyo wao wote.


Nao walikuwa wakijitoa kufuata mafundisho ya mitume, kuishi katika ushirika wa kindugu, kumega mukate na kuomba.


Milango ya kuingilia katika muji wa Yeriko ilikuwa imefungwa imara kwa ndani kwa kuwazuia Waisraeli wasiingie. Hakuna mutu aliyeweza kuingia wala kutoka katika muji huo.


Wakati ule Yoshua akaapa mbele ya watu akisema: “Atakayeujenga tena muji wa Yeriko, alaaniwe na Mungu. Yeyote atakayeweka musingi wa muji huo, muzaliwa wake wa kwanza akufe. Yeyote atakayejenga mulango wa muji huo, mwana wake kitenda mimba akufe.”


Lakini Ruta akamujibu: “Usinisihi nikuache wewe, wala usinizuie kufuatana nawe. Popote utakapokwenda ndipo nami nitakapokwenda, na pale utakapokaa mimi nitakaa, watu wako watakuwa watu wangu, na Mungu wako atakuwa Mungu wangu.


Hana akamwambia: “Ee bwana wangu, kama vile unavyoishi, bwana wangu, mimi ni yule mwanamuke aliyekuwa anasimama mbele yako akimwomba Yawe.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ