Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Wafalme 2:23 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

23 Elisha aliondoka Yeriko, akaenda Beteli. Alipokuwa katika njia, vijana wamoja walitoka katika muji, wakaanza kumuzomea wakisema: “Kwenda zako, kwenda zako muzee wa upaa!”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Wafalme 2:23
34 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini wao waliendelea kuwachekelea wajumbe wa Mungu, wakayazarau maneno yake na kuwachekelea manabii wake mpaka kwa mwisho kasirani ya Yawe ikawaka juu ya watu wake hata hakukukuwa wa kuwaponyesha.


Lakini sasa watu wananichekelea, tena watu wanaokuwa wadogo kuliko mimi; watu ambao niliwaona baba zao hawafai hata kuwahesabu kama imbwa wangu wakilinda kondoo.


Hata watoto wadogo wananizarau; wakati ninapojitokeza wao wananizomea.


Usiniache nifezeheke, ee Yawe, maana mimi ninakulilia; lakini uwaache waovu wafezeheke, uwaache wapotelee huko kuzimu.


Wengine walichekelewa na kupigwa fimbo, na wengine walifungwa minyororo na kutupwa katika kifungo.


Zamani mutoto aliyezaliwa sawa kawaida alimutesa yule aliyezaliwa kwa uwezo wa Roho wa Mungu, na ingali inafanyika vile hata sasa.


Usitoe tena unabii hapa katika Beteli, kwa sababu hapa ni pahali ya ibada ya mufalme; ni hekalu la utawala huu.


Lakini musinitafutie kule Beteli wala musiende Gilgali wala musivuke kwenda Beri-Seba. Maana wakaaji wa Gilgali, hakika watapelekwa katika uhamisho, na Beteli utaangamizwa!


Enyi Waisraeli, muende basi kule Beteli na kuniasi! Muende Gilgali muongeze makosa yenu! Mutoe sadaka zenu kila asubui na zaka zenu kwa siku ya tatu.


Siku nitakapowaazibu Waisraeli kwa sababu ya makosa yao, nitayaharibu vilevile mazabahu ya muji wa Beteli. Nitazikata pembe za kila mazabahu na kuziangusha chini.


Ndivyo itakavyokuwa kwenu enyi watu wa Beteli, kwa sababu ya uovu wenu mukubwa. Kutakapopambazuka mufalme wa Israeli atauawa.


Wakaaji wa Samaria watatetemeka kwa sababu ya sanamu ya mwana-ngombe wa kule Beteli. Watu wake watamwombolezea mwana-ngombe yule, hata makuhani wanaomwabudu watamulilia; maana utukufu wa mwana-ngombe yule umeondolewa.


Ikiwa kweli ninyi Waisraeli ni wazinzi lakini, watu wa Yuda basi wasianguke ndani ya makosa! Musiende pahali patakatifu kule Gilgali, wala musiende kule Nyumba ya Uovu. Wala musiape mukisema: Kama vile Yawe anavyoishi!


Watoto wanaokota kuni, wababa wanawakisha moto na wamama wanaponda unga kwa ajili ya kutengeneza mikate ya kumutambikia mungu wa kike, wanayemwita malkia wa mbinguni. Tena wananikasirikisha kwa kuitolea miungu mingine sadaka ya divai.


Watu watatesana, kila mutu na mwenzake; vijana watawazarau wazee, na watu wa ovyo ovyo watawazarau wenye heshima.


Ole kwako wewe taifa lenye zambi, watu waliolemewa na uovu, kizazi cha watenda mabaya, watoto wanaoishi kwa udanganyifu! Ninyi mumemwacha Yawe, mumemuzarau Mutakatifu wa Israeli, mumerudi nyuma.


Ondoa mahangaiko ndani ya moyo wako, ujikinge usipate maumivu katika mwili kwa sababu ujana na nguvu vinapita mbio.


Ujinga umefungwa ndani ya moyo wa mutoto, lakini fimbo ya kufundisha itaufukuza mbali.


Umufundishe mutoto njia anayopaswa kufuata, naye hataiacha hata katika uzee.


Hata mutoto anajulikana kwa matendo yake, kama ni safi na sawa.


Lakini mimi nilipoanguka, walikusanyika kunisimanga. Walikusanyika kuniuzi. Wageni nisiowajua walinizomea bila kukoma, wala hakuna aliyewazuia.


Siku moja Sara akamwona Isimaeli, mutoto wa Abrahamu aliyezaliwa na Hagari Mumisri, akicheza na Isaka mwana wake.


Walipokuwa wanatembea na kuongea, kwa rafla gari la moto lililokokotwa na farasi wa moto likawatenganisha. Naye Elia akanyanyuliwa mbinguni katika upepo wa kuzungukazunguka.


Kama mwanaume amepata upaa, yeye ni safi maana ana upaa tu.


Na maji hayo yakakuwa ya kufaa mpaka leo, kama vile Elisha alivyosema.


Uniangalie mimi mutumishi wako; uniokoe kwa wema wako.


Walipokuwa katika njia, Elia akamwambia Elisha: “Tafazali ubakie hapa. Yawe amenituma niende Beteli.” Lakini Elisha akamwambia: “Kama vile Yawe anavyoishi na kama vile unavyoishi, sitakuacha.” Basi, wakaenda pamoja mpaka Beteli.


Ee Yawe, wewe umenidanganya, nami kweli nimedanganyika; wewe una nguvu kuliko mimi, nawe umeshinda. Nimekuwa mutu wa kuchekelewa kila siku, kila mutu ananizarau.


Kila mara ninaposema kitu, ninalalamika, ninapandisha sauti kwa kutangaza mateso na uharibifu. Kutangaza neno la Yawe kunaniletea kuzomewa na kuzarauliwa kila siku.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ