Lakini wao walimwuzi sana mpaka akaona haya, akawaambia: “Muwatume.” Hivyo wakawatuma watu makumi tano, wakaenda wakamutafuta kila fasi kwa muda wa siku tatu nao hawakumwona.
Kisha watu wa Yeriko wakamwendea Elisha, wakamwambia: “Bwana, kama vile unavyoona, muji huu ni muzuri, lakini maji tunayokuwa nayo ni mabaya na yanasababisha mimba kuharibika.”