Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Wafalme 2:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Wakamwambia: “Sisi watumishi wako tuko na mashujaa makumi tano. Tafazali, uwaruhusu waende kumutafuta bwana wako. Labda roho wa Yawe amemubeba na kumutupa juu ya mulima fulani au katika bonde.” Elisha akajibu: “Hapana, musiwatume.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Wafalme 2:16
8 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ninaogopa kwamba mara tu nitakapoondoka, Roho wa Yawe atakunyanyua na kukupeleka pahali nisipopajua! Nikienda kumwambia Ahabu kwamba uko hapa, naye akikutafuta na asikupate, ataniua mimi, ingawa mimi mutumishi wako ninamwogopa Yawe tangu ujana wangu.


Manabii makumi tano wakawafuata mpaka kwenye muto Yordani. Elia na Elisha wakasimama karibu na muto, nao manabii wakasimama mbali kidogo.


Nikiwa katika maono hayo, Roho wa Mungu alininyanyua na kunipeleka mpaka katika inchi ya Babeli, kwa watu wanaokuwa kule katika uhamisho. Kisha maono hayo yakatoweka.


Basi, Roho akaninyanyua juu na kunipeleka mbali. Yawe alinijaza uwezo wake. Nami nikaenda nikiwa na uchungu na hasira katika roho yangu.


Basi, nikiwa katika maono Yawe akanipeleka mpaka katika inchi ya Israeli, akaniweka juu ya mulima murefu sana, na upande wa kusini kulikuwa majengo yaliyoonekana kama muji.


Basi, akanyoosha kitu kinachokuwa kama vile mukono, akanikamatia kwa nywele zangu. Roho wa Mungu akaninyanyua kati ya dunia na mbingu, akanipeleka mpaka Yerusalema nikiwa katika maono hayo ya Mungu. Nikafika kwenye kiingilio cha mulango wa baraza ya ndani inayoelekea upande wa kaskazini, pahali palipowekwa sanamu iliyomuletea Mungu wivu.


Walipotoka ndani ya maji, kwa rafla Roho wa Bwana akamutowesha Filipo, na yule mukubwa hakumwona tena, lakini akaongeza safari yake katika furaha.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ