2 Wafalme 2:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
1 Wakati ulifika ambapo Yawe alitaka kumupandisha Elia mbinguni katika upepo wa kuzungukazunguka. Elia na Elisha walikuwa katika njia, wakitoka Gilgali.
Ninaogopa kwamba mara tu nitakapoondoka, Roho wa Yawe atakunyanyua na kukupeleka pahali nisipopajua! Nikienda kumwambia Ahabu kwamba uko hapa, naye akikutafuta na asikupate, ataniua mimi, ingawa mimi mutumishi wako ninamwogopa Yawe tangu ujana wangu.
Yawe akamwambia: “Kwenda usimame juu ya mulima, mbele yangu mimi Yawe.” Basi, Yawe akapita na kuuvumisha upepo mukali ambao uliporomosha milima na kuvunja mawe makubwa. Lakini Yawe hakukuwa katika upepo ule. Upepo ukapita, kukakuwa tetemeko la inchi. Lakini Yawe hakukuwa katika tetemeko la inchi.
naye akatembea mwendo wa siku nzima kuingia katika jangwa. Basi, akafika, akaikaa chini ya muti mumoja wa muretemu. Halafu, akaomba apate kufa, akisema: “Inatosha! Siwezi tena. Ee Yawe, sasa utoe uzima wangu. Mimi si bora kuliko babu zangu.”
Walipokuwa wanatembea na kuongea, kwa rafla gari la moto lililokokotwa na farasi wa moto likawatenganisha. Naye Elia akanyanyuliwa mbinguni katika upepo wa kuzungukazunguka.
Elisha akarudi Gilgali wakati katika inchi kulikuwa njaa. Siku moja, alipokuwa akifundisha wanafunzi wa manabii alimwambia mutumishi wake: “Weka chungu kikubwa juu ya moto, uwapikie manabii chakula.”
Kwa njia ya imani, Enoki alibebwa na Mungu toka katika dunia pasipo kufa. Naye hakuonekana tena, kwa sababu Mungu alimubeba mbinguni. Maana Maandiko Matakatifu yanasema kwamba mbele ya kubebwa kwake, Enoki alishuhudiwa kwamba alimupendeza Mungu.