Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Wafalme 18:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Aliharibu nafasi zote za kuabudu miungu na kuvunja nguzo na kukata Ashera. Vilevile, alivunja nyoka ya shaba ambayo Musa alitengeneza, iliyoitwa Nehustani. Mpaka wakati ule, watu wa Israeli walikuwa wakiitambikia.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Wafalme 18:4
30 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Alitenda mema mbele ya Yawe kama vile baba yake Asa alivyofanya.


na kutoa nguzo takatifu na kuiteketeza kwa moto.


Halafu wakaaji wakaenda kwenye nyumba ya Bali na kuibomoa, wakavunja mazabahu pamoja na sanamu zake, hata wakamwua Matani, kuhani wa Bali mbele ya mazabahu. Kuhani Yehoyada akaweka walinzi kwa kulinda nyumba ya Yawe.


Wakati wa maisha yake yote alitenda kwa usawa mbele ya Yawe, kwa sababu kuhani Yehoyada alikuwa akimufundisha.


Nafasi za kutambikia kwenye milima hazikuharibiwa na watu waliendelea kutambika na kufukiza ubani kwa nafasi zile.


Hata hivyo, nafasi za kutambikia miungu ya uongo hazikuharibiwa, na watu waliendelea kutambikia na kufukiza ubani kwenye nafasi za juu. Yotamu alijenga mulango wa kaskazini wa nyumba ya Yawe.


Hata hivyo, nafasi za kutambikia kwenye milima hazikuharibiwa, na watu waliendelea kutambika na kufukiza ubani pale.


Kisha alimwamuru Uria: “Tumia hii mazabahu yangu kubwa kwa kuteketeza sadaka za asubui na sadaka za unga za magaribi, sadaka za kuteketezwa, sadaka za unga za mufalme na za watu wote na vilevile sadaka za divai za watu. Unyunyize damu ya nyama wote wa kuteketezwa ambao wametolewa sadaka. Lakini ile mazabahu ya shaba nitaitumia mimi kwa kuuliza shauri toka kwa Mungu.”


Lakini hata kama mukiniambia: ‘Tunamutegemea Yawe, Mungu wetu’, si huyohuyo ambaye Hezekia aliziharibu nafasi zake zote za kuabudu kwenye vilima pamoja na mazabahu zake na kuwaambia watu wa Yuda na Yerusalema: Munapaswa kuabudu mbele ya mazabahu hii ya Yerusalema tu?


Alitengeneza upya nafasi za kuabudia miungu mingine zilizoharibiwa na baba yake Hezekia. Akajenga mazabahu za kuabudia Bali na kutengeneza sanamu ya Ashera, kama vile Ahabu mufalme wa Israeli alivyofanya. Vilevile, Manase aliabudu na kutumikia jeshi la mbingu.


Alivunja nguzo vipandevipande; vilevile alikatakata sanamu za Ashera, na pahali zilipokuwa zinasimama akapajaza mifupa ya watu.


Kisha Yosia akaamuru Kuhani Mukubwa Hilkia na makuhani wasaidizi wake na walinzi wa mulango watoe katika hekalu la Yawe vitu vilivyotengenezwa kwa ajili ya Bali, Ashera na kwa ajili ya jeshi la mbingu. Aliviteketeza inje ya Yerusalema katika bonde la Kidroni na kupeleka majivu yake kule Beteli.


Lakini, kuna wema fulani ndani yako. Umekwisha kuondoa sanamu zote za Ashera, mungu wa kike, na umejikaza sana kumutafuta Mungu kwa moyo wote.”


Nyuma ya sherehe kumalizika, watu wote wa Israeli wakakwenda katika kila muji wa Yuda, wakavunjavunja nguzo za mawe na kukatakata sanamu za Ashera, mungu wa kike, na vilevile wakaharibu mazabahu na pahali pa kuabudia miungu mingine. Wakafanya vile katika inchi yote ya Yuda, Benjamina, Efuraimu na Manase, mpaka walipokwisha kuvimaliza vyote. Kisha Waisraeli wakarudi kwao, kila mutu kwenye urizi wake.


Kwa maana alijenga tena pahali pa kuabudia miungu mingine palipokuwa pamebomolewa na baba yake Hezekia; akajenga mazabahu za kuabudia Mabali, na kutengeneza sanamu za Ashera. Vilevile, aliabudu jeshi la mbinguni na kulitumikia.


Walimukasirikisha kwa mazabahu zao za miungu; wakamutia wivu kwa sanamu zao za kuchongwa.


Musiiname mbele ya miungu yao kuiabudu, wala kuitumikia, wala musiige mambo yao. Lakini mutawaangamiza kabisa na kuvunjavunja nguzo zao.


Lakini mutabomoa mazabahu zao na kuvunja nguzo zao za ibada na sanamu zao za Ashera.


Lakini hata kama mukiniambia ‘Tunamutegemea Yawe, Mungu wetu’, si huyohuyo ambaye Hezekia aliziharibu nafasi zake zote za kuabudu kwenye vilima pamoja na mazabahu zake na kuwaambia watu wa Yuda na Yerusalema: Munapaswa kuabudu mbele ya mazabahu hii ya Yerusalema tu?


Nitaharibu pahali penu pa ibada kule juu ya milima, nitabomoa mazabahu zenu za kufukizia ubani, na kutupa maiti zenu juu ya sanamu za miungu yenu. Roho yangu itawachukia kabisa.


Wakati huo mimi nikasimama kati yenu na Yawe, nikawatangazia yale aliyosema, kwa sababu ninyi muliogopa ule moto na hamukupanda juu ya mulima. Yawe akasema hivi:


Lakini muwatendee hivi: Mutavunja mazabahu zao na kubomoa nguzo zao. Na sanamu za Ashera mutakata na kuchoma sanamu zao za kuchonga.


Usiku ule, Yawe akamwambia Gideoni: “Twaa ngombe dume mumoja wa baba yako, ngombe dume yule wa pili wa umri wa miaka saba. Bomoa mazabahu ya mungu Bali baba yako anayokuwa nayo na kuvunja sanamu ya mungu Ashera inayokuwa karibu nayo.


Wakaaji wa muji walipoamuka asubui mapema waliona mazabahu ya Bali na sanamu ya Ashera iliyokuwa karibu nayo vimeharibiwa. Yule ngombe dume wa pili alikuwa ameteketezwa juu ya mazabahu iliyokuwa imejengwa pahali pale.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ