Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Wafalme 17:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 na kufuata njia za mataifa ambayo Yawe aliyafukuza wakati watu wake walipokuwa wanaingia, na kufanya matendo ya wafalme wa Israeli waliyoyaingiza katika inchi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Wafalme 17:8
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, kisha kushauriana na wengine, akatengeneza sanamu mbili za zahabu. Kisha akawaambia watu: “Enyi watu wa Israeli, hii ndiyo miungu yenu iliyowatoa katika inchi ya Misri! Hakuna sababu ya kwenda Yerusalema kutoa sadaka kule.”


Alitenda machukizo kwa kuabudu sanamu za miungu kama vile Waamori walivyofanya ambao zamani Yawe aliwafukuza mbele ya watu wa Israeli.


Mufalme Ahazi alipokwenda Damasiki kukutana na mufalme Tigilati-Pileseri, aliona mazabahu kule. Basi, akamutumia kuhani Uria mufano kamili na muchoro wa mazabahu hiyo.


lakini alifuata mwenendo wa wafalme wa Israeli. Akamutambikia hata mwana wake kwa kuteketezwa kwa moto, akifuata desturi mbaya za mataifa ambayo yalifukuzwa na Yawe wakati Waisraeli walipokuwa wanaingia katika inchi.


Lakini hata watu wa Yuda hawakutii amri za Yawe, Mungu wao; lakini walifuata desturi zilizoletwa na watu wa Israeli.


Lakini watu hao hawakusikiliza, wao waliendelea kutenda kama vile walivyofanya zamani.


Alitenda maovu mbele ya Yawe kwa kutenda maovu ya mataifa ambayo yalifukuzwa na Yawe mbele ya watu wa Israeli.


Lakini walichanganyika na watu wa mataifa, wakajifunza kutenda mambo yao.


Musiiname mbele ya miungu yao kuiabudu, wala kuitumikia, wala musiige mambo yao. Lakini mutawaangamiza kabisa na kuvunjavunja nguzo zao.


Yawe anasema hivi: Musiige mwenendo wa mataifa mengine, wala musishangazwe na vitambulisho vya ajabu munavyoviona katika mbingu; muyaache mataifa mengine yashangazwe navyo.


Lakini wakaaji wake wameyaasi maagizo na masharti yangu, wakakuwa wabaya kuliko mataifa na inchi zinazowazunguka. Kweli, wameyakataa maagizo yangu na kuacha kuyafuata masharti yangu.


Efuraimu ameteswa, haki zake zimetwaliwa; maana alikusudia kufuata mambo isiyokuwa na maana.


Musifanye kama vile watu wa inchi ya Misri ambako mulikaa wanavyofanya, wala musifanye kama vile watu wa inchi ya Kanana ambako ninawapeleka wanavyofanya. Musifuate desturi zao hata kidogo.


Musijitengenezee sanamu za miungu ya uongo, musishike sanamu zao za kuchongwa wala nguzo wala sanamu za mawe yaliyochongwa katika inchi yenu na kuviabudu. Mimi ni Yawe, Mungu wenu.


Ninyi munafuata mufano mubaya wa mufalme Omuri na mufano mubaya wa jamaa ya mwana wake, Ahabu, na mumefuata mashauri yao. Kwa hiyo nitawaletea maangamizi, na kila mutu atawazarau. Watu watawachekelea kila pahali.


“Mutakapofika katika ile inchi Yawe, Mungu wenu, anayowapa, musifuate zile tabia za kuchukiza za mataifa ya huko.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ