Lakini wakati mumoja Hoshea alituma wajumbe kwa mufalme wa Misri akiomba musaada; ndipo akaacha kulipa kodi kwa mufalme Salmanaseri wa Asuria kama vile alivyozoea kufanya kila mwaka. Salmanaseri alipoona hivi alimufunga Hoshea kwa minyororo na kumuweka katika kifungo.
Katika mwaka wa ine wa utawala wa Hezekia, ambao vilevile ulikuwa mwaka wa saba wa utawala wa Hoshea mwana wa Ela mufalme wa Israeli, Salmanaseri mufalme wa Asuria alishambulia muji wa Samaria na kuuzunguka.