Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Wafalme 17:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Lakini wakati mumoja Hoshea alituma wajumbe kwa mufalme wa Misri akiomba musaada; ndipo akaacha kulipa kodi kwa mufalme Salmanaseri wa Asuria kama vile alivyozoea kufanya kila mwaka. Salmanaseri alipoona hivi alimufunga Hoshea kwa minyororo na kumuweka katika kifungo.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Wafalme 17:4
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mufalme Salmanaseri wa Asuria alimushambulia; naye Hoshea akakuwa mutumishi wake na kumulipa kodi.


Kisha mufalme wa Asuria akashambulia inchi nzima na kuufikia muji wa Samaria na kuuzunguka kwa muda wa miaka mitatu.


Angalia sasa. Unategemea Misri, utete uliovunjika ambao utamuchoma mukono mutu yeyote atakayeutegemea. Hivi ndivyo mufalme wa Misri anavyokuwa kwa wote wale wanaomutegemea.


Nebukadneza mufalme wa Babeli akaishambulia inchi ya Yuda. Yoyakimu akamutumikia kwa miaka mitatu halafu akaacha kumutii, akamwasi.


Yawe aliwakasirikia sana watu wa Yerusalema na Yuda, hata akawafukuza mbali naye. Zedekia alimwasi mufalme wa Babeli.


Halafu wakawaua wana wa Zedekia mbele yake, kisha wakamwongoa macho yake. Kwa mwisho wakamufunga kwa minyororo, wakamupeleka Babeli.


Si Hezekia ndiye anayewadanganya mukufe kwa njaa au kiu anapowaambia: ‘Yawe, Mungu wenu atawaokoa toka mikono ya mufalme wa Asuria?’


Wanachosema ni maneno matupu; wanaapa na kufanya mapatano ya bure; haki imekuwa si haki tena, inachipuka kama mimea yenye sumu katika shamba.


Watu wa Efuraimu wanachunga upepo, muchana kutwa wanafukuza upepo wa mashariki. Wanazidisha uongo na mateso, wanafanya mapatano na Asuria na kupeleka mafuta Misri.


Yuko wapi sasa mufalme wenu awaokoe? Wako wapi wale wakubwa wenu wawalinde? Ninyi ndio mulioomba: Utupatie mufalme na wakubwa watutawale.


Wametafuta wapenzi kati ya watu wa mataifa, lakini mimi nitawakusanya. Na hapo watasikia uzito wa muzigo wa mufalme wa wakubwa.


“Yawe atawapeleka ninyi na mufalme wenu mutakayejichagulia, mpaka kwa taifa ambalo ninyi hamukulijua wala wazee wenu. Na huko mutatumikia miungu mingine ya miti na mawe.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ