Kisha aliwashinda Wamoabu. Aliwapanga katika mistari mateka hao, na kuwalalisha chini. Aliamuru wale waliokuwa katika mistari miwili wauawe na wale wa mustari wa tatu waachwe wazima. Hivyo, Wamoabu wakakuwa watumishi wa Daudi na wakakuwa wanamulipa kodi.
Halafu Daudi aliweka kambi za waaskari katika muji wa Waaramu wa Damasiki. Basi, Waaramu wakakuwa watumishi wake na wakakuwa wanamulipa kodi. Yawe alimupa Daudi ushindi kokote alikokwenda.
Basi, Puli mufalme wa Asuria akashambulia inchi ya Israeli, naye Menahemu akamupa kilo elfu makumi tatu na ine za feza kusudi amusaidie kuimarisha mamlaka yake juu ya inchi ya Israeli.
Menahemu alipata feza hiyo kwa kuwalazimisha watajiri wa Israeli kutoa muchango wa vikoroti makumi tano vya feza kila mumoja. Halafu Puli hakukaa Israeli lakini akarudi katika inchi yake.
Wakati wa utawala wa Peka mufalme wa Israeli, Tigilati-Pileseri, mufalme wa Asuria, aliteka miji ya Iyoni, Abeli-Beti-Maka, Yanoa, Kadesi na Hazori, pamoja na inchi za Gileadi, Galilaya na Nafutali na kuwahamisha wakaaji wake kwenda Asuria.
Lakini wakati mumoja Hoshea alituma wajumbe kwa mufalme wa Misri akiomba musaada; ndipo akaacha kulipa kodi kwa mufalme Salmanaseri wa Asuria kama vile alivyozoea kufanya kila mwaka. Salmanaseri alipoona hivi alimufunga Hoshea kwa minyororo na kumuweka katika kifungo.
Musimusikilize Hezekia, maana mufalme wa Asuria anasema: ‘Mukuwe na amani nami na kujitoa kwangu. Kisha kila mumoja wenu ataweza kula matunda ya mizabibu yake mwenyewe na matunda ya tini yake mwenyewe na kunywa maji ya kisima chake mwenyewe,
Kwa hiyo, ee Mungu wetu, Mungu mukubwa, mwenye nguvu na wa kutisha, wewe unashika agano lako na kutenda wema. Mateso yaliyotupata, sisi, wafalme wetu, wakubwa wetu, makuhani wetu, manabii wetu, babu zetu na watu wako wote tangu wakati wa wafalme wa Asuria mpaka leo, usiyaone kuwa ni madogo.
Kwa hiyo fujo ya vita itawafikia watu wako, kuta zako zote zitaharibiwa. Kama vile mufalme Salmani alivyoharibu Beti-Arbeli katika vita, wamama wakapondwa pamoja na watoto wao.
Nitawaletea upanga ambao utalipiza kisasi juu ya agano mulilovunja. Ninyi mutakimbilia katika miji yenu, lakini nitawaletea ugonjwa mukali na kuwatia katika mikono ya waadui zenu.