Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Wafalme 16:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 lakini alifuata mwenendo wa wafalme wa Israeli. Akamutambikia hata mwana wake kwa kuteketezwa kwa moto, akifuata desturi mbaya za mataifa ambayo yalifukuzwa na Yawe wakati Waisraeli walipokuwa wanaingia katika inchi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Wafalme 16:3
32 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kukakuwa hata ibada za uasherati katika inchi, nao walitenda matendo ya kuchukiza, sawasawa na yale matendo ya mataifa ambayo Mungu aliyafukuza mbele ya Waisraeli.


Walivunja amri zote za Yawe, Mungu wao. Wakatengeneza sanamu za miungu ya wana-ngombe wawili wa madini yenye kuyeyushwa, wakatengeneza sanamu za Ashera, wakaabudu jeshi la mbingu, na wakamutumikia Bali.


Waliwatambikia watoto wao wa kiume na wa kike kwa miungu ya uongo; wakaomba shauri kwa watabiri na wachawi. Walijitoa kabisa kutenda maovu mbele ya Yawe, wakamukasirikisha sana.


Lakini hata watu wa Yuda hawakutii amri za Yawe, Mungu wao; lakini walifuata desturi zilizoletwa na watu wa Israeli.


na kufuata njia za mataifa ambayo Yawe aliyafukuza wakati watu wake walipokuwa wanaingia, na kufanya matendo ya wafalme wa Israeli waliyoyaingiza katika inchi.


“Kwa sababu mufalme amefanya mambo ya kuchukiza, mambo mabaya zaidi ya yale yaliyotendwa na Waamori waliomutangulia, akawasukuma watu wa Yuda vilevile watende zambi kwa kutumia sanamu zake,


Alitenda maovu mbele ya Yawe kwa kutenda maovu ya mataifa ambayo yalifukuzwa na Yawe mbele ya watu wa Israeli.


Naye alimutoa mwana wake kama sadaka ya kuteketezwa kwa moto. Alipiga ramuli; aliaguza akishirikiana na waaguzi wanaosemezana na mizimu na wachawi. Alitenda maovu mengi mbele ya Yawe, akamukasirikisha.


Lakini hawakusikia, naye Manase aliwasukuma watende zambi zaidi kuliko zile zilizofanywa na mataifa ambayo Yawe aliyaharibu mbele ya Waisraeli.


Mufalme Yosia aliharibu pahali pa kuabudia miungu ya uongo palipoitwa Tofeti katika bonde la wana wa Hinomu, kusudi mutu yeyote asimuteketeze mwana wake au binti yake kama sadaka kwa Moleki.


Alifuata mwenendo wa wafalme wa Israeli, kama vile jamaa ya Ahabu ilivyofanya, kwa sababu muke wake alikuwa binti ya Ahabu. Akatenda maovu mbele ya Yawe.


Kwa sababu mama yake alikuwa mushauri wake katika kutenda maovu, naye vilevile alifuata mienendo ya jamaa ya Ahabu.


Alitenda maovu mbele ya Yawe kwa kuiga mienendo miovu ya mataifa ambayo Yawe aliyafukuza wakati watu wake wa Israeli walipokuwa wanaingia.


Na aliwatoa wana wake kama sadaka ya kuteketezwa kwa moto katika bonde la mwana wa Hinomu. Alipiga ramuli, aliaguza na alitumia hirizi; hata alishirikiana na waaguzi wanaosemezana na mizimu na wachawi. Alitenda maovu mengi mbele ya Yawe, akamukasirikisha.


Lakini walichanganyika na watu wa mataifa, wakajifunza kutenda mambo yao.


Ninyi munawaka tamaa kwenye miti ya mialo, na chini ya kila muti wenye kuwa na majani mabichi. Munawachinja watoto wenu na kuwatambikia katika mabonde na ndani ya nyufa za mawe.


Walimujengea mungu Bali mazabahu katika bonde la Mwana wa Hinomu, kusudi wamutolee mungu Moleki wana wao na wabinti zao, ingawa sikuwaamuru wala sikufikiria kwamba wangefanya hivyo. Wakasukuma watu wa Yuda watende zambi.


Jambo hili la kuwachinja watoto wangu kwa kuwa sadaka ya kuteketeza kwa ajili ya sanamu zako ni jambo dogo?


Lakini wewe haukutosheka kufuata mienendo yao au kutenda sawa na machukizo yao. Kwa muda mufupi tu ulipotoka kuliko vile wao walivyopotoka katika mienendo yako yote.


Nikawaacha wajichafue kwa sadaka zao za kuwatoa wazaliwa wao wa kwanza sadaka ya kuteketezwa kwa moto. Hili lilikuwa pigo lao la azabu ya kutisha kusudi watambue kwamba mimi ni Yawe.


Munapoendelea kutoa sadaka zenu na kuwateketeza watoto wenu kwa moto munajichafua mpaka leo hii. Nitaulizwa shauri nanyi, enyi watu wa Israeli? Kama vile ninavyoishi, –ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe– sitakubali kuulizwa shauri nanyi.


Usimutoe mutoto wako yeyote kuwa sadaka kwa mungu Moleki maana kufanya hivyo utazarau jina langu mimi Mungu wako. Mimi ni Yawe.


Uwaambie Waisraeli hivi: Mutu yeyote kati ya Waisraeli au mugeni anayekaa kati yenu, akimutoa mutoto wake yeyote kuwa sadaka kwa mungu Moleki, mutu huyu anapaswa kuuawa. Wanainchi wa pale watamwua kwa kumupiga mawe.


Yawe atapendezwa nikimutolea maelfu ya kondoo dume, au mito elfu na elfu ya mafuta? Nimutolee muzaliwa wangu wa kwanza kwa ajili ya kosa langu, mutoto wangu wa kwanza kwa ajili ya zambi yangu?


Musimwabudu Yawe, Mungu wenu, hivyo, kwa maana kila chukizo ambalo Yawe hapendi, wameifanyia miungu yao, hata wamewachoma ndani ya moto watoto wao wanaume na wanawake, kwa kutambikia miungu yao.


Kusikuwe mutu yeyote kati yenu anayemupitisha kwenye moto mutoto wake mwanaume au mwanamuke kuwa tambiko, wala mutu anayepiga ramuli, wala mwaguzi, wala mwenye kufanya uganga,


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ