Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Wafalme 15:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Katika mwaka wa makumi tatu na nane wa utawala wa Azaria mufalme wa Yuda, Zakaria mwana wa Yeroboamu akaanza kutawala Israeli. Akatawala kwa muda wa miezi sita.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Wafalme 15:8
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yawe akamwambia Yehu: “Umewatendea wazao wa Ahabu yale yote niliyotaka uwatendee. Kwa hiyo nimekuahidi kwamba wazao wako mpaka kizazi cha ine watatawala Israeli.”


Kisha watu wote wa Yuda wakamukamata Azaria akiwa na umri wa miaka kumi na sita, wakamufanya kuwa mufalme kwa pahali pa Amazia baba yake.


Yeroboamu akakufa na kuzikwa katika makaburi ya kifalme na mwana wake Zakaria akatawala kwa pahali pake.


Katika mwaka wa makumi mbili na saba wa kutawala kwa Yeroboamu mufalme wa Israeli, Azaria mwana wa Amazia, mufalme wa Yuda, akaanza kutawala.


Katika mwaka wa makumi tatu na tisa wa utawala wa mufalme Azaria wa Yuda, Salumu mwana wa Yabesi akaanza kutawala Israeli na akatawala akiwa kule Samaria kwa muda wa mwezi mumoja.


Katika mwaka wa makumi tatu na tisa wa utawala wa mufalme Azaria wa Yuda, Menahemu mwana wa Gadi akaanza kutawala Israeli. Akatawala akiwa kule Samaria kwa muda wa miaka kumi.


Katika mwaka wa makumi tano wa utawala wa mufalme Azaria wa Yuda, Pekahia mwana wa Menahemu akaanza kutawala Israeli. Akatawala akiwa kule Samaria kwa muda wa miaka miwili.


Azaria akakufa na kuzikwa katika makaburi ya wafalme katika muji wa Daudi; na mwana wake Yotamu akatawala kwa pahali pake.


Naye, kama vile watangulizi wake, alitenda maovu mbele ya Yawe; hakuacha zambi zile za Yeroboamu mwana wa Nebati ambaye aliwasukuma watu wa Israeli watende zambi.


Taifa lenye fujo lina viongozi wengi, lakini kwa kiongozi mumoja mwenye akili na maarifa kuna utengemano.


Yawe akamwambia Hosea: Umupange mutoto huyo jina la “Yezereheli”, maana kisha siku chache tu, nitaiazibu jamaa ya Yehu kwa mauaji aliyofanya katika bonde la Yezereheli. Hivi nitavunja ufalme katika taifa la Israeli.


Kule kwenye vilima ambapo wazao wa Isaka wanatambikia, kutafanywa kuwa uharibifu mutupu na mahekalu ya Waisraeli yatakuwa mabomoko. Nitaushambulia kwa vita ukoo wa mufalme Yeroboamu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ