2 Wafalme 15:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
8 Katika mwaka wa makumi tatu na nane wa utawala wa Azaria mufalme wa Yuda, Zakaria mwana wa Yeroboamu akaanza kutawala Israeli. Akatawala kwa muda wa miezi sita.
Yawe akamwambia Yehu: “Umewatendea wazao wa Ahabu yale yote niliyotaka uwatendee. Kwa hiyo nimekuahidi kwamba wazao wako mpaka kizazi cha ine watatawala Israeli.”
Katika mwaka wa makumi tatu na tisa wa utawala wa mufalme Azaria wa Yuda, Salumu mwana wa Yabesi akaanza kutawala Israeli na akatawala akiwa kule Samaria kwa muda wa mwezi mumoja.
Katika mwaka wa makumi tatu na tisa wa utawala wa mufalme Azaria wa Yuda, Menahemu mwana wa Gadi akaanza kutawala Israeli. Akatawala akiwa kule Samaria kwa muda wa miaka kumi.
Katika mwaka wa makumi tano wa utawala wa mufalme Azaria wa Yuda, Pekahia mwana wa Menahemu akaanza kutawala Israeli. Akatawala akiwa kule Samaria kwa muda wa miaka miwili.
Naye, kama vile watangulizi wake, alitenda maovu mbele ya Yawe; hakuacha zambi zile za Yeroboamu mwana wa Nebati ambaye aliwasukuma watu wa Israeli watende zambi.
Yawe akamwambia Hosea: Umupange mutoto huyo jina la “Yezereheli”, maana kisha siku chache tu, nitaiazibu jamaa ya Yehu kwa mauaji aliyofanya katika bonde la Yezereheli. Hivi nitavunja ufalme katika taifa la Israeli.
Kule kwenye vilima ambapo wazao wa Isaka wanatambikia, kutafanywa kuwa uharibifu mutupu na mahekalu ya Waisraeli yatakuwa mabomoko. Nitaushambulia kwa vita ukoo wa mufalme Yeroboamu.