Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Wafalme 15:23 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

23 Katika mwaka wa makumi tano wa utawala wa mufalme Azaria wa Yuda, Pekahia mwana wa Menahemu akaanza kutawala Israeli. Akatawala akiwa kule Samaria kwa muda wa miaka miwili.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Wafalme 15:23
10 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Katika mwaka wa pili wa utawala wa Asa kule Yuda, Nadabu mwana wa Yeroboamu alianza kutawala katika inchi ya Israeli. Alitawala kwa muda wa miaka miwili.


Katika mwaka wa makumi mbili na sita wa utawala wa Asa mufalme wa Yuda, Ela mwana wa Basha alianza kutawala kule Israeli akiwa Tirza. Alitawala kwa muda wa miaka miwili.


Kwa mwisho, Yosafati akakufa, akazikwa pamoja na babu zake katika makaburi ya kifalme katika muji wa Daudi babu yake. Naye Yoramu mwana wake akatawala kwa pahali pake.


Katika mwaka wa makumi mbili na saba wa kutawala kwa Yeroboamu mufalme wa Israeli, Azaria mwana wa Amazia, mufalme wa Yuda, akaanza kutawala.


Menahemu akakufa, naye mwana wake Pekahia akatawala kwa pahali pake.


Alitenda maovu mbele ya Yawe; hakuacha zambi za Yeroboamu mwana wa Nebati ambaye aliwasukuma watu wa Israeli watende zambi.


Katika mwaka wa makumi tano na mbili wa utawala wa mufalme Azaria wa Yuda, Peka mwana wa Remalia akaanza kutawala akiwa kule Samaria kwa muda wa miaka makumi mbili.


Katika mwaka wa makumi tatu na nane wa utawala wa Azaria mufalme wa Yuda, Zakaria mwana wa Yeroboamu akaanza kutawala Israeli. Akatawala kwa muda wa miezi sita.


Amoni alikuwa na umri wa miaka makumi mbili na mbili alipoanza kutawala, akatawala miaka miwili akiwa kule Yerusalema. Jina la mama yake ni Mesulemeti binti ya Haruzi, wa muji Yotibati.


mwovu atajiona ameshinda kwa muda tu, furaha ya asiyemwogopa Mungu ni ya muda mufupi tu!


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ