22 Menahemu akakufa, naye mwana wake Pekahia akatawala kwa pahali pake.
Salumu mwana wa Yabesi alimwasi, akamupiga mbele ya watu na kumwua, kisha akatawala kwa pahali pake.
Mambo mengine ya Menahemu na yote aliyofanya yameandikwa katika Kitabu cha Mambo ya Siku za Wafalme wa Israeli.
Katika mwaka wa makumi tano wa utawala wa mufalme Azaria wa Yuda, Pekahia mwana wa Menahemu akaanza kutawala Israeli. Akatawala akiwa kule Samaria kwa muda wa miaka miwili.