Mungu akamusikia mutoto yule akilia, na malaika wa Mungu akamwita Hagari kutoka mbinguni, akamwambia: “Una shida gani Hagari? Usiogope. Mungu amesikia sauti ya mutoto kule anapokuwa.
Kama Mungu wa babu yangu Abrahamu, Mungu ambaye ni kitisho cha Isaka, asingelikuwa upande wangu, hakika ungeliniacha niondoke mikono mitupu. Lakini Mungu aliona mateso yangu na kazi niliyofanya kwa mikono yangu, akakukaripia usiku wa kuamukia leo.”
Lakini Yawe aliwarehemu na kuwaonea huruma. Aliwaangalia kwa wema kwa sababu ya agano lake na Abrahamu, Isaka na Yakobo. Hakuwaangamiza wala hajawaachilia hata kidogo mpaka leo.
Maombi yake na jinsi Mungu alivyomupokea, zambi zake zote na ukosefu wa uaminifu kwake, pahali alipojenga pa kutambikia na jinsi alivyotengeneza sanamu za Ashera na sanamu zingine mbele ya kujinyenyekeza, vimeandikwa katika Kitabu cha Mambo ya Waonaji.
Kisha Yawe akamwambia: “Nimeona mateso ya watu wangu wanaokuwa katika inchi ya Misri na nimesikia kilio chao kinachosababishwa na watesaji wao. Ninajua mateso yao,
Katika taabu zao zote, hakumutuma mujumbe mwingine kwa kuwasaidia, lakini yeye mwenyewe alikuja kuwaokoa; kwa upendo na huruma yake aliwakomboa. Aliwabeba na kuwakamata tangu zamani.
Wao wanauambia muti: “Wewe ni baba yetu”, nalo jiwe: “Wewe ndiwe uliyetuzaa”; kwa maana unanigeuzia mugongo, wala hawakunielekezea uso. Lakini wakati wa shida wanasema: Simama utuokoe!
Basi, watu wakamwendea Musa, wakamwambia: Tumetenda zambi kwa kumunungunikia Yawe na wewe vilevile. Umwombe Yawe atuondolee nyoka hawa. Kwa hiyo, Musa akawaombea watu.