Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Wafalme 13:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Yoahazi akamusihi Yawe, naye Yawe alipoona jinsi mufalme wa Aramu alivyowatesa watu wa Israeli akasikia maombi yake.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Wafalme 13:4
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mungu akamusikia mutoto yule akilia, na malaika wa Mungu akamwita Hagari kutoka mbinguni, akamwambia: “Una shida gani Hagari? Usiogope. Mungu amesikia sauti ya mutoto kule anapokuwa.


Kama Mungu wa babu yangu Abrahamu, Mungu ambaye ni kitisho cha Isaka, asingelikuwa upande wangu, hakika ungeliniacha niondoke mikono mitupu. Lakini Mungu aliona mateso yangu na kazi niliyofanya kwa mikono yangu, akakukaripia usiku wa kuamukia leo.”


Mufalme Hazaeli wa Aramu akawatesa sana watu wa Israeli wakati wote wa utawala wa Yoahazi.


Lakini Yawe aliwarehemu na kuwaonea huruma. Aliwaangalia kwa wema kwa sababu ya agano lake na Abrahamu, Isaka na Yakobo. Hakuwaangamiza wala hajawaachilia hata kidogo mpaka leo.


Ni kwa sababu Yawe aliona taabu kubwa Waisraeli waliyopata maana hakukuwa mutu yeyote wa kuwasaidia.


Maombi yake na jinsi Mungu alivyomupokea, zambi zake zote na ukosefu wa uaminifu kwake, pahali alipojenga pa kutambikia na jinsi alivyotengeneza sanamu za Ashera na sanamu zingine mbele ya kujinyenyekeza, vimeandikwa katika Kitabu cha Mambo ya Waonaji.


Kwa hiyo tukafunga na kumwomba Mungu atulinde, naye akayasikia maombi yetu.


Utamwomba naye atakusikiliza, nawe utavitimiza viapo vyako.


Uniite wakati wa taabu, nami nitakuokoa, nawe utanitukuza.”


Kila mara alipowaua, waliobaki walimugeukia; wakageuka toka ubaya wao, wakamugeukia Mungu kwa moyo.


Kisha Yawe akamwambia: “Nimeona mateso ya watu wangu wanaokuwa katika inchi ya Misri na nimesikia kilio chao kinachosababishwa na watesaji wao. Ninajua mateso yao,


Hakika, kilio cha Waisraeli kimenifikia; nimeona jinsi Wamisri wanavyowatesa.


Ee Yawe, walipotaabika walikutafuta, walikuomba musaada ulipowaazibu.


Katika taabu zao zote, hakumutuma mujumbe mwingine kwa kuwasaidia, lakini yeye mwenyewe alikuja kuwaokoa; kwa upendo na huruma yake aliwakomboa. Aliwabeba na kuwakamata tangu zamani.


Wao wanauambia muti: “Wewe ni baba yetu”, nalo jiwe: “Wewe ndiwe uliyetuzaa”; kwa maana unanigeuzia mugongo, wala hawakunielekezea uso. Lakini wakati wa shida wanasema: Simama utuokoe!


Uniite, nami nitakujibu na kukuambia mambo makubwa yaliyofichwa ambayo haujapata kuyajua.


Basi, watu wakamwendea Musa, wakamwambia: Tumetenda zambi kwa kumunungunikia Yawe na wewe vilevile. Umwombe Yawe atuondolee nyoka hawa. Kwa hiyo, Musa akawaombea watu.


Basi wakamulilia Yawe, wakisema: “Tumetenda zambi mbele yako, maana tumekuacha wewe Mungu wetu, tukatumikia Mabali.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ