Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Wafalme 13:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Alitenda maovu mbele ya Yawe. Alitenda zambi sawa na Yeroboamu mwana wa Nebati ambaye aliwasukuma watu wa Israeli watende zambi. Hakuacha kutenda zambi hii.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Wafalme 13:2
8 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yawe ataitupilia Israeli kwa sababu ya zambi za Yeroboamu ambaye alitenda zambi na kuwasukuma watu wa Israeli vilevile watende zambi.”


Lakini hakuacha zambi zile za Yeroboamu mwana wa Nebati ambaye aliwasukuma Waisraeli watende zambi, ni kusema ile ibada ya sanamu za wana-ngombe wa zahabu kule Beteli na Dani.


Katika mwaka wa makumi mbili na tatu wa utawala wa mufalme Yoasi wa Yuda, Yoahazi mwana wa Yehu alianza kutawala Israeli, akaendelea kutawala akiwa kule Samaria kwa muda wa miaka kumi na saba.


Yoasi vilevile alitenda maovu mbele ya Yawe. Hakuacha zambi zile za Yeroboamu mwana wa Nebati ambaye aliwasukuma watu wa Israeli watende zambi. Aliendelea kuzitenda.


Hata hivyo hawakuacha zambi za mufalme Yeroboamu ambaye aliwasukuma watu wa Israeli watende zambi; lakini waliendelea na zambi zao na sanamu ya Ashera ilibakia kule Samaria.


Hata hivyo, Yoramu aliendelea kutenda zambi ileile ya Yeroboamu mwana wa Nebati ambaye aliwasukuma watu wa Israeli watende zambi. Hakuiacha.


Efuraimu ameteswa, haki zake zimetwaliwa; maana alikusudia kufuata mambo isiyokuwa na maana.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ