Mufalme alifuata maagizo ya nabii na kufungua dirisha ambalo lilielekea Aramu. Elisha akatoa amri: “Tupa mushale!” Mara tu mufalme alipotupa mushale, nabii akasema: “Wewe ndio mushale wa Yawe, ambao kwa njia yake atapata ushindi juu ya Waaramu. Utapigana na Waaramu kule Afeki mpaka uwashinde.”
Halafu akajilaza juu ya mutoto, kinywa chake juu ya kinywa cha mutoto, na macho yake juu ya macho ya mutoto na mikono yake juu ya mikono ya mutoto. Na alipokuwa amekaa hivyo, mwili wa mutoto ukaanza kupata joto.