Kwa hiyo mufalme Yoasi alimwita kuhani Yehoyada na makuhani wengine na kuwauliza: “Mbona hamujatengeneza nyumba? Basi, sasa hamutapokea tena feza kutoka kwa wengine lakini zitaletwa kusudi nyumba itengenezwe.”
Kisha Yosia akaamuru Kuhani Mukubwa Hilkia na makuhani wasaidizi wake na walinzi wa mulango watoe katika hekalu la Yawe vitu vilivyotengenezwa kwa ajili ya Bali, Ashera na kwa ajili ya jeshi la mbingu. Aliviteketeza inje ya Yerusalema katika bonde la Kidroni na kupeleka majivu yake kule Beteli.
Kisha Nebuzaradani mukubwa wa waaskari walinzi wa mufalme akamupeleka Seraya, Kuhani Mukubwa, kuwa mufungwa pamoja na Zefania, kuhani wa pili, na wakubwa wa walinda milango watatu.
Kisha wakawachagua Walawi hawa wakuwe wasaidizi wao kwa kushika nafasi ya pili: Zekaria, Yazieli, Semiramoti, Yehieli, Uni, Eliabu, Benaya, Maseya, Matitia, Elifelehu na Mikineya na walinzi wa mulango: Obedi-Edomu na Yeieli.
Sebania, Yosafati, Netaneli, Amasai, Zekaria, Benaya na Eliezeri, waliokuwa makuhani, waliwekwa kwa kupiga baragumu mbele ya Sanduku la Agano. Obedi-Edomu na Yehiya waliwekwa vilevile kuwa walinzi wa sanduku.
nikawaleta kwenye nyumba ya Yawe, katika chumba cha wana wa mutu wa Mungu Hanani mwana wa Igidalia. Chumba hicho kilikuwa karibu na chumba cha wakubwa juu ya chumba cha mulinzi wa mulango Maseya mwana wa Salumu.
Kisha Nebuzaradani mukubwa wa waaskari walinzi wa mufalme, alimukamata Seraya Kuhani Mukubwa, na Zefania kuhani wa pili, pamoja na walinda mulango watatu;
Yesu akaikaa akielekea kwenye sanduku ya kutilia sadaka za hekalu. Akaangalia jinsi watu walivyotia feza ndani ya sanduku ile. Watajiri wengi walitia feza nyingi ndani yake.