Katika mwaka wa saba wa utawala ya mufalme Yehu wa Israeli, Yoasi alianza kutawala Yuda kule Yerusalema, naye akatawala kwa muda wa miaka makumi ine akiwa kule Yerusalema. Mama yake aliitwa Sibia wa Beri-Seba.
Hata hivyo, nafasi za kutambikia miungu ya uongo hazikuharibiwa, na watu waliendelea kutambikia na kufukiza ubani kwenye nafasi za juu. Yotamu alijenga mulango wa kaskazini wa nyumba ya Yawe.
Aliharibu nafasi zote za kuabudu miungu na kuvunja nguzo na kukata Ashera. Vilevile, alivunja nyoka ya shaba ambayo Musa alitengeneza, iliyoitwa Nehustani. Mpaka wakati ule, watu wa Israeli walikuwa wakiitambikia.
Zaidi ya hayo, mufalme akawaambia wakaaji wa Yerusalema watoe sehemu makuhani na Walawi waliyostahili kupewa, kusudi wao wajitolee kikamilifu katika shuguli za sheria za Yawe.
Yawe anasema: Tangu zamani wewe ulivunja nira yako, ulikata minyororo yako, ukasema: “Sitakutumikia”. Juu ya kila kilima kirefu na chini ya kila muti wa majani mabichi, ukalala machali kama kahaba.