Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Wafalme 12:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Wakati wa maisha yake yote alitenda kwa usawa mbele ya Yawe, kwa sababu kuhani Yehoyada alikuwa akimufundisha.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Wafalme 12:3
13 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mufalme Asa alitenda mambo yanayokuwa mema mbele ya Yawe kama vile Daudi babu yake alivyofanya.


Lakini nafasi ya kutambikia miungu juu ya vilima haikuharibiwa. Hata hivyo, yeye alikuwa na moyo mwaminifu kwa Yawe maisha yake yote.


Alitenda mema mbele ya Yawe kama vile baba yake Asa alivyofanya.


Katika mwaka wa saba wa utawala ya mufalme Yehu wa Israeli, Yoasi alianza kutawala Yuda kule Yerusalema, naye akatawala kwa muda wa miaka makumi ine akiwa kule Yerusalema. Mama yake aliitwa Sibia wa Beri-Seba.


Nafasi za kutambikia kwenye milima hazikuharibiwa na watu waliendelea kutambika na kufukiza ubani kwa nafasi zile.


Alitenda kwa usawa mbele ya Yawe kama vile baba yake Amazia alivyotenda.


Hata hivyo, nafasi za kutambikia miungu ya uongo hazikuharibiwa, na watu waliendelea kutambikia na kufukiza ubani kwenye nafasi za juu. Yotamu alijenga mulango wa kaskazini wa nyumba ya Yawe.


Hata hivyo, nafasi za kutambikia kwenye milima hazikuharibiwa, na watu waliendelea kutambika na kufukiza ubani pale.


Alitenda kwa usawa mbele ya Yawe, kama vile Daudi babu yake alivyotenda.


Aliharibu nafasi zote za kuabudu miungu na kuvunja nguzo na kukata Ashera. Vilevile, alivunja nyoka ya shaba ambayo Musa alitengeneza, iliyoitwa Nehustani. Mpaka wakati ule, watu wa Israeli walikuwa wakiitambikia.


Yosia alitenda kwa usawa mbele ya Yawe. Alifuata mienendo yote ya babu yake Daudi; hakuiacha hata kidogo.


Zaidi ya hayo, mufalme akawaambia wakaaji wa Yerusalema watoe sehemu makuhani na Walawi waliyostahili kupewa, kusudi wao wajitolee kikamilifu katika shuguli za sheria za Yawe.


Yawe anasema: Tangu zamani wewe ulivunja nira yako, ulikata minyororo yako, ukasema: “Sitakutumikia”. Juu ya kila kilima kirefu na chini ya kila muti wa majani mabichi, ukalala machali kama kahaba.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ