Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Wafalme 10:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Asubui yake akatoka, akasimama na kuwaambia watu wote: “Ninyi ni watu wa haki. Mimi nilifanya mupango wa kuasi bwana wangu na kumwua. Lakini ni nani aliyewaua hawa wote?

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Wafalme 10:9
7 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yehu akawaandikia barua ingine akiwaambia: “Ikiwa kweli muko tayari kufuata maagizo yangu, mulete hapa Yezereheli vichwa vya wana wa bwana wenu nivipate kesho kwa wakati kama huu.” Wana makumi saba wa mufalme Ahabu waliishi kwa viongozi wa Samaria, ambao walikuwa walezi wao.


Kisha mutumishi mumoja akamwendea na kusema: “Vichwa vya wana wa mufalme vimekwisha kuletwa.” Halafu akaamuru: “Muviweke chini katika mafungu mawili kwenye mulango wa muji, muviache vikae kule mpaka asubui.”


Wakubwa wa serikali yake wakamwasi, wakamwuia katika uwanja wa Milo kwenye barabara inayoelekea Sila.


Kwa hiyo rafiki yangu anasema hivi: Enyi wakaaji wa Yerusalema na watu wa Yuda, tafazali mukuwe waamuzi kati yangu na shamba langu.


Yawe akamwambia Hosea: Umupange mutoto huyo jina la “Yezereheli”, maana kisha siku chache tu, nitaiazibu jamaa ya Yehu kwa mauaji aliyofanya katika bonde la Yezereheli. Hivi nitavunja ufalme katika taifa la Israeli.


Niko hapa, na kama nimefanya tendo lolote baya, basi, mutoe ushuhuda mbele ya Yawe na mbele ya mufalme wake muchaguliwa. Nimenyanganya ngombe dume au punda wa mutu yeyote? Nimemugandamiza mutu yeyote? Nimemutesa mutu yeyote? Nimepokea kituliro kwa mutu yeyote kusudi nifunge macho mbele ya matendo yake? Museme nami nitamurudishia kitu chochote kile.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ