2 Wafalme 10:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
7 Basi, barua ilipowafikia, waliwatwaa hao wana wa mufalme na kuwakata vichwa wote makumi saba. Waliweka vichwa vyao katika vikapu na kumupelekea Yehu kule Yezereheli.
Umwambie, Yawe anasema hivi: ‘Umeua na kutwaa mali yake vilevile?’ Umwambie Yawe anasema hivi: ‘Pahali pale imbwa walipoilambulia damu ya Naboti, ndipo watakapoilambulia damu yako.’ ”
Basi! Yawe anasema hivi: ‘Hakika, nitakuletea maangamizi. Nitakuletea hasa wewe na kuangamiza kila mwanaume wa ukoo wako katika Israeli, akuwe mutumwa au huru.
Yehu akawaandikia barua ingine akiwaambia: “Ikiwa kweli muko tayari kufuata maagizo yangu, mulete hapa Yezereheli vichwa vya wana wa bwana wenu nivipate kesho kwa wakati kama huu.” Wana makumi saba wa mufalme Ahabu waliishi kwa viongozi wa Samaria, ambao walikuwa walezi wao.
Kisha mutumishi mumoja akamwendea na kusema: “Vichwa vya wana wa mufalme vimekwisha kuletwa.” Halafu akaamuru: “Muviweke chini katika mafungu mawili kwenye mulango wa muji, muviache vikae kule mpaka asubui.”
Asubui yake akatoka, akasimama na kuwaambia watu wote: “Ninyi ni watu wa haki. Mimi nilifanya mupango wa kuasi bwana wangu na kumwua. Lakini ni nani aliyewaua hawa wote?
Yoramu alipoikalia kiti cha kifalme na utawala wake ulipokuwa umekwisha kuimarika, yeye akawaua wandugu zake wote kwa upanga, na vilevile wakubwa wamoja wa Israeli.