Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Wafalme 1:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Halafu akamutuma kiongozi mumoja wa waaskari na watu wake makumi tano wamulete Elia. Kiongozi huyo akaenda, akamukuta Elia akiikaa kwenye mulima, akamwambia: “Ewe mutu wa Mungu, mufalme anakuamuru ushuke.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Wafalme 1:9
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yule mwanamuke akamwambia Elia: “Ewe mutu wa Mungu, kuna maneno gani kati yako nami? Kumbe ulikuja kwangu kwa kuzifichua zambi zangu na kusababisha kifo cha mwana wangu?”


Ninakuapia kwa jina la Yawe, Mungu wako, Mwenye Uzima, kwamba mufalme amekuwa akikutafuta katika dunia yote. Na mufalme yeyote akisema kwamba haujaonekana kule, Ahabu alimutaka huyo mufalme aape na watu wake kwamba kweli hauko.


na wakati Yezebeli alipowaua manabii wa Yawe, Obadia aliwachukua manabii mia moja, akawaficha makumi tano tano ndani ya pango, akakuwa anawapelekea chakula na maji.


Basi, Ahabu akaenda zake kula na kunywa. Naye Elia akapanda juu ya kilele cha mulima Karmeli, na kule akainama uso mpaka chini na kuuweka uso wake katikati ya magoti yake.


Yezebeli akatuma mujumbe kwa Elia amwambie: “Miungu waniue, ninakuapia, kama kesho nisipokuua kwa wakati kama huu sawa vile ulivyowaua wale manabii.”


Naye mufalme wa Israeli akamujibu Yosafati: “Kungali mumoja, Mikaya mwana wa Imula. Yeye tunaweza kumwomba shauri la Yawe. Lakini ninamuchukia sana kwa sababu yeye, hatabiri jambo zuri juu yangu hata kidogo, lakini baya tu.” Yosafati akamwambia: “Si vizuri kwa mufalme kusema hivyo.”


Elisha akaendelea na safari yake mpaka kwenye mulima Karmeli na tokea kule akarudi Samaria.


Basi, akaondoka, akaenda mpaka kwenye mulima Karmeli kule mutu wa Mungu alipokuwa. Mutu wa Mungu alipomwona akikuja, akamwambia Gehazi mutumishi wake: “Angalia, ninamwona Musunami akikuja.


nikawaleta kwenye nyumba ya Yawe, katika chumba cha wana wa mutu wa Mungu Hanani mwana wa Igidalia. Chumba hicho kilikuwa karibu na chumba cha wakubwa juu ya chumba cha mulinzi wa mulango Maseya mwana wa Salumu.


Kisha Amazia akamwambia Amosi: Sasa tumechoka nawe, ewe nabii! Uende! Urudie katika inchi ya Yuda, utoe unabii kule upate na chakula chako kulekule.


Herode alikuwa amemukamata Yoane akamufunga minyororo na kumutia ndani ya kifungo. Herode alifanya vile kwa sababu ya Herodia, muke wa ndugu yake Filipo.


wakisema: “Ewe Kristo, tambua ni nani aliyekupiga!”


Nao wakasokota taji na tawi lenye miiba na kumuvalisha nalo kwenye kichwa chake. Wakaweka tete katika mukono wake wa kuume, wakapiga magoti mbele yake na kumuchekelea, wakisema: “Jambo, Mufalme wa Wayuda!”


Watu waliokuwa wakipita pale walimutukana na kutikisatikisa vichwa vyao, wakisema: “Ewe! Wewe uliyetaka kubomoa hekalu na kujenga lingine katika siku tatu,


Kristo, Mufalme wa Waisraeli, ajishushe sasa juu ya musalaba, kusudi nasi tupate kuona na kumwamini.” Hata wale waliotundikwa pamoja naye walimutukana vilevile.


Wanafunzi wake, Yakobo na Yoane walipoona mambo hayo, wakasema: “Bwana, unataka tuombe moto uwashukie toka mbinguni na kuwateketeza?”


Wengine walichekelewa na kupigwa fimbo, na wengine walifungwa minyororo na kutupwa katika kifungo.


Saulo alipopata habari zile, alituma watumishi wengine, nao vilevile wakaanza kutabiri. Saulo akatuma watumishi wengine kwa mara ya tatu, nao vilevile wakaanza kutabiri.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ