Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Wafalme 1:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Lakini malaika wa Yawe akamwambia nabii Elia wa muji wa Tisibe, aende kukutana na wajumbe hao na kuwauliza: “Kwa nini munakwenda kwa Bali-Zebubu, mungu wa Ekuroni? Hakuna Mungu katika inchi ya Israeli?

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Wafalme 1:3
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nitafanya hivyo kwa sababu Solomono ameniacha, akaabudu miungu ya kigeni: Astaroti mungu wa Wasidoni, Kemosi mungu wa Wamoabu, na Milkomu mungu wa Waamoni. Solomono ameniasi, ametenda maovu mbele yangu. Hakutii masharti yangu na maagizo yangu kama Daudi baba yake alivyofanya.


Basi Elia wa kijiji cha Tisibe katika jimbo la Gileadi akamwambia mufalme Ahabu: “Kama vile Yawe, Mungu wa Israeli, ambaye ninamutumikia, anavyoishi, hakutakuwa umande wala mvua mpaka nitakapotoa amri.”


Nyuma ya siku nyingi, katika mwaka wa tatu wa ukosefu wa mvua, neno la Yawe lilimufikia Elia kusema hivi: “Kwenda ujionyeshe kwa mufalme Ahabu, halafu nitanyesha mvua katika inchi.”


Kwa wakati wa kutoa sadaka ya magaribi, nabii Elia aliikaribia mazabahu, akaomba: “Ee Yawe, Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo, uwaonyeshe watu leo hii kwamba wewe ndiwe Mungu wa Israeli, na kwamba mimi ni mutumishi wako na nimefanya mambo haya kwa amri yako.


Basi, Elia akalala chini ya muti ule, akashikwa na usingizi. Kisha muda kidogo, malaika akakuja, akamugusa na kumwambia: “Amuka ukule.”


Malaika wa Yawe akamufikia tena kwa mara ya pili, akamugusa na kumwambia: “Amuka ukule, kama sivyo safari itakuwa ngumu sana kwako.”


Basi, neno la Yawe lilimufikia Elia wa Tisibe kusema hivi:


Mufalme Ahazia alipokuwa Samaria alianguka kutoka chumba kilichokuwa juu ya paa ya nyumba yake, akaumia vibaya. Kwa hiyo akawatuma wajumbe, akawaambia: “Muende kwa Bali-Zebubu, mungu wa muji wa Ekuroni, mumwulize kama nitapona ugonjwa huu.”


Wakamujibu: “Tumekutana na mutu ambaye alitutuma turudi kukuambia kwamba Yawe amesema hivi: ‘Kwa nini unatuma wajumbe kwa Bali-Zebubu, mungu wa Ekuroni? Hakuna Mungu katika inchi ya Israeli? Hautashuka katika kitanda ulichopanda juu yake. Hakika utakufa.’ ”


Wao wakamujibu: “Alikuwa akivaa nguo ya manyoya na mukaba wa ngozi kwenye kiuno.” Mufalme akasema: “Yule ni Elia wa Tisibe!”


Halafu akarudi kwa mutu wa Mungu pamoja na watu wake, akasema: “Sasa ninajua kwamba hakuna Mungu yeyote katika dunia lakini tu Mungu wa Israeli; kwa hiyo, tafazali sasa upokee zawadi ya mutumishi wako.”


Elisha, nabii wa Mungu, alipopata habari kwamba mufalme wa Israeli amepasua nguo zake, alituma ujumbe kwa mufalme, akamwuliza: “Kwa sababu gani umepasua nguo zako? Umutume mutu huyo kwangu, kusudi apate kujua kwamba kuna nabii katika Israeli!”


Kwa mukubwa wa waimbaji: kwa vyombo vyenye nyuzi. Zaburi ya Asafu. Wimbo.


Watu wamoja watawaambia ninyi: Muombe shauri kwa mizimu na waaguzi wanaolia kama ndege; kwa sababu ni kawaida watu kuomba shauri kwa miungu yao, na kuomba shauri kwa wafu kwa ajili ya wanaokuwa wazima.


Roho yangu ilipoanza kunitoka, nilikukumbuka, ee Yawe, maombi yangu yakakufikia katika hekalu lako takatifu.


Walimu wa Sheria waliotoka Yerusalema, wakasema hivi juu ya Yesu: “Amepatwa na Belzebuli.” Na wengine wao wakasema: “Ni huyo mukubwa wa pepo ndiye anayemupa uwezo wa kufukuza pepo.”


Malaika wa Bwana akamwambia Filipo: “Ujitayarishe na uende upande wa kusini kupitia njia inayotelemuka toka Yerusalema kwenda katika muji Gaza, nayo ni njia watu wasiyozoea kupitia.”


Siku ya leo, Yawe atakutia katika mikono yangu. Nitakushinda, nitakukata kichwa chako; na miili ya waaskari wa Wafilistini nitawapa ndege na nyama wa pori. Halafu dunia nzima itajua kwamba Mungu yuko katika Israeli.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ