Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Timoteo 4:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Watafunga masikio yao wasisikilize mambo ya kweli na kusikiliza hadisi za uongo.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Timoteo 4:4
13 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Maana wajinga wanajiua kwa kiburi chao, wapumbafu wanajiangamiza kwa kufanikiwa kwao.


Wanawaambia wale wanaopata maono hivi: Musipate maono. Wanawaambia manabii hivi: Musitutangazie ukweli, lakini mutuambie mambo ya kupendeza, mutoe unabii wa mambo ya udanganyifu tu.


Lakini watu walikataa kunisikiliza, waligeuza mabega na kuziba masikio yao kusudi wasisikie.


Maana mioyo ya watu hawa imegeuka migumu, wameziba masikio yao, nao wamefunga macho yao, kusudi wasipate kuona, nao wasipate kusikia, wala wasipate kunigeukia, nami ningewaponyesha.’


Basi wale wajumbe wakafunga masikio yao, wakapiga kelele kwa nguvu na kumurukia wote pamoja.


Kwa sababu hii Mungu amewaweka chini ya nguvu ya upotovu wapate kuamini mambo ya uongo.


Uwaambie wasishikamane na hadisi za uongo, pamoja na mambo yasiyokuwa na mwisho ya wababu. Hayo yote yanaleta mabishano, wala hayafai kitu kwa kutimiza mupango wa Mungu wa wokovu, unaojulikana kwa njia ya imani.


Lakini ukatae hadisi za uongo zilizotungwa na wanawake wazee. Ujizoeze katika maisha yako kumwabudu Mungu kwa ukweli.


Timoteo, uchunge vizuri kile ulichopewa kwa kulinda, ukiepuka maneno ya kidunia na mabishano yasiyokuwa na maana juu ya ile watu wengine wanayoita kuwa ni elimu lakini ni uongo.


Kama unavyojua wewe mwenyewe, watu wote wa jimbo la Azia wameniacha; kati yao kuna Figelo na Hermogene.


Na zaidi ya ile hawatafuata hadisi za uongo za Kiyuda wala maagizo ya watu waliopotoka mbali na ukweli.


Basi, wakati tulipowajulisha uwezo na kurudia kwa Bwana wetu Yesu Kristo, sisi hatukutumia hadisi za uongo zilizotungwa kwa werevu. Lakini tulijionea na macho yetu sisi wenyewe uwezo wake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ