Nao walipofika katika muji Salami, wakahubiri Neno la Mungu katika nyumba za kuabudia za Wayuda. Yoane alikuwa pamoja nao, akiwasaidia kwa kufanya kazi.
Siku ya Sabato ilipotimia tukatoka ndani ya muji ule na kwenda karibu na muto mumoja, kwenye nafasi tulipozania kuwa ya kufanyia maombi. Tukaikaa na kusemezana na wanawake waliokusanyika pale.
Siku ya kwanza ya juma, tulikuwa tunakusanyika kwa kumega mukate. Paulo akasemezana na watu na kuendelea kuwahubiria mpaka katikati ya usiku, kwa sababu alikusudia kuondoka kesho yake.
Na namna gani watahubiri ikiwa hawatumwi? Ni kama inavyoandikwa katika Maandiko Matakatifu: “Angalia jinsi kunavyofurahisha kuja kwa wale wanaoleta habari njema.”
Mutuombee sisi vilevile kusudi Mungu atufungulie njia ya kuhubiri neno lake tupate kutangaza ujumbe wa siri juu ya Kristo. Ni kwa ajili ya ujumbe ule mimi niko sasa katika kifungo.
Basi kama mutu atajitakasa kwa kujitenga na maovu hayo yote atakuwa chombo cha matumizi ya kipekee, kitakatifu cha mwenye nyumba na chenye mafaa kwake na kuwa tayari kwa kila kazi njema.
Lakini wewe umefuata kabisa mufano wangu katika mafundisho yangu na mwenendo wangu, makusudi yangu, imani yangu, uvumilivu wangu, upendo wangu, ungojevu wangu,