Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Timoteo 4:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 utangaze Neno la Mungu kwa nguvu kwa wakati unaofaa na kwa wakati usiofaa. Ukaripe, usahihishe na kuonya ukifundisha kwa uvumilivu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Timoteo 4:2
36 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ninataka kutimiza mapenzi yako, ee Mungu wangu; sheria yako ninaishika kwa moyo wangu wote!”


Simama, uende Ninawe, ule muji mukubwa, uwatangazie watu ujumbe ninaokupa.


Heri mutu yule ambaye sitakuwa kikwazo kwake.”


Wale wasimamizi walipofika kwa Yesu, wakamusihi sana, wakasema: “Umufanyie mutu huyu sawa anavyokuomba, kwa maana anastahili kutendewa vile.


Yesu akamwambia: “Uwaache hao wafu wazike wafu wao, lakini wewe uende kutangaza habari ya Ufalme wa Mungu.”


Nao walipofika katika muji Salami, wakahubiri Neno la Mungu katika nyumba za kuabudia za Wayuda. Yoane alikuwa pamoja nao, akiwasaidia kwa kufanya kazi.


Siku ya Sabato ilipotimia tukatoka ndani ya muji ule na kwenda karibu na muto mumoja, kwenye nafasi tulipozania kuwa ya kufanyia maombi. Tukaikaa na kusemezana na wanawake waliokusanyika pale.


Siku ya kwanza ya juma, tulikuwa tunakusanyika kwa kumega mukate. Paulo akasemezana na watu na kuendelea kuwahubiria mpaka katikati ya usiku, kwa sababu alikusudia kuondoka kesho yake.


Tulipofika Roma, Paulo akapewa ruhusa ya kujilipia nyumba ya kupanga ambamo atakaa pamoja na askari mumoja mwenye kumuchunga.


Na namna gani watahubiri ikiwa hawatumwi? Ni kama inavyoandikwa katika Maandiko Matakatifu: “Angalia jinsi kunavyofurahisha kuja kwa wale wanaoleta habari njema.”


Mufurahi mukiwa na tumaini, muvumilie katika mateso, mudumu katika kuomba.


Mwenye kufundishwa Habari Njema anapaswa kushirikiana mapato yake na yule anayemufundisha.


Mimi nimekuwa mutumishi wa kanisa kufuatana na kazi ile Mungu aliyonipa kwa ajili yenu. Kazi yenyewe ni kutangaza Neno lake kwa ukamilifu.


Mutuombee sisi vilevile kusudi Mungu atufungulie njia ya kuhubiri neno lake tupate kutangaza ujumbe wa siri juu ya Kristo. Ni kwa ajili ya ujumbe ule mimi niko sasa katika kifungo.


Ninyi mumefuata mufano wetu na mufano wa Bwana, kwa kuwa ingawa muliteswa sana, mulipokea neno la Mungu kwa furaha inayotoka kwa Roho Mutakatifu.


Tunawasihi wandugu, muwaonye wale wanaokuwa wavivu, muwatie moyo wale wanaoregea, muwasaidie wale wanaokuwa zaifu, na mukuwe wavumilivu kwa watu wote.


Kwa kungojea mpaka nitakapofika, ujitolee kwa kuwasomea watu Maandiko Matakatifu kwa kuwaonya na kuwafundisha.


Wale wenye kufanya zambi, uwakaripie mbele ya watu kusudi wengine wapate kuogopa vilevile.


Basi kama mutu atajitakasa kwa kujitenga na maovu hayo yote atakuwa chombo cha matumizi ya kipekee, kitakatifu cha mwenye nyumba na chenye mafaa kwake na kuwa tayari kwa kila kazi njema.


Anapaswa kuwaonya kwa upole wale wanaopingana naye; kwa maana labda Mungu anaweza kuwajalia hata wapate kugeuka toka zambi na kutambua ukweli.


Lakini wewe umefuata kabisa mufano wangu katika mafundisho yangu na mwenendo wangu, makusudi yangu, imani yangu, uvumilivu wangu, upendo wangu, ungojevu wangu,


Ushuhuda huo ni wa kweli. Basi kwa hiyo uwaonye vikali, kusudi wapate kuwa na imani kamili.


Haya ndiyo maneno unayopaswa kufundisha, ukiwaonya watu na kuwakaripia kwa mamlaka yote. Usijiachilie kuzarauliwa na mutu yeyote.


Wandugu, ninawasihi kupokea kwa uvumilivu haya maonyo ninayowatolea kwa maana nimewaandikia kwa kifupi.


Mimi ninawaonya na kuwaazibu wote ninaowapenda. Basi ufanye nguvu, ugeuke toka katika zambi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ