Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Timoteo 3:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Hawatakuwa na upendo wala huruma. Watakuwa wenye kusingiziana, wasiojizuiza, wakali na wasiopenda mema.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Timoteo 3:3
31 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ninalaani hasira yao kali sana na kasirani yao isiyokuwa na huruma. Nitawatawanya katika inchi ya Yakobo, nitawasambaza katika inchi ya Israeli.


Walikulilia wewe, wakaokolewa; walikutegemea, nao hawakufezeheka.


Alizarauliwa na kukataliwa na watu. Alikuwa mutu wa uchungu na huzuni. Alikuwa kama mutu wa kuchukiza kwa watu; alizarauliwa na tukamwona si kitu.


Wazao wa wale waliokutesa, watakuja na kuinama uso mpaka chini mbele yako. Wote wale waliokuzarau, watapiga magoti kwenye miguu yako. Watakuita: “Muji wa Yawe”, “Sayuni”, “Muji wa Mutakatifu wa Israeli”.


Wakati falme hizo zitakapofikia kwa mwisho wao na uovu wao kufikia kilele chake, kutatokea mufalme mumoja mutesaji na mwerevu.


“Ndugu atamutoa ndugu, kusudi auawe, na baba atamutoa mutoto wake, nao watoto watawageukia wazazi wao na kuwaua.


Kisha Roho Mutakatifu akamwongoza Yesu kwenda katika jangwa kusudi ajaribiwe na Shetani.


Yesu akaongeza kuwaambia wanafunzi wake: “Yule anayewasikiliza ninyi, ananisikiliza mimi; yule asiyewapokea ninyi, hanipokei mimi, na yule asiyenipokea mimi, hamupokei yule aliyenituma.”


Wakati Wafarisayo waliposikia maneno haya yote wakamuzarau Yesu, kwa sababu walikuwa wapenda feza.


Yesu akawajibu: “Ni mimi peke niliyewachagua ninyi kumi na wawili, lakini ingawa hivi mumoja wenu ni Shetani!”


Wamejaa kila namna ya uovu, ubaya, tamaa na upotovu. Wamejaa wivu, uuaji, ugomvi, udanganyifu na ukorofi. Wao ni wenye kuchongeana,


hawana zamiri, hawawezi kuaminiwa, hawana upendo wala huruma.


Musinyimane, isipokuwa tu mumepatana na kwa muda tu kusudi mupate wakati wa kujitoa kwa kufunga na kuomba. Kisha munaweza kurudiliana tena kusudi Shetani asiwajaribu katika uzaifu wenu.


Lakini kama hawawezi kujizuiza wao wenyewe, basi waoane; kwa maana afazali kuoa kuliko kuwaka tamaa.


Basi kwa hiyo, yeye anayekataa mafundisho haya hamukatai mutu, lakini anamukataa Mungu anayewapa ninyi Roho wake Mutakatifu.


Wanawake wao wanapaswa kuwa na adabu vilevile, wasikuwe wasingiziaji wa uongo, lakini wakuwe wakadirifu na waaminifu katika mambo yote.


Lakini inafaa akuwe mwenye kupenda kukaribisha wageni, mwenye kupenda mema, mukadirifu, mwenye haki, mutakatifu na mutaratibu.


Vilevile uwaambie wanawake wazee wakuwe na mwenendo unaostahili kwa watu watakatifu. Hawapaswi kuwa wasingiziaji, wala wasikuwe watumwa wa pombe, lakini wakuwe wenye kutoa mafundisho mazuri.


Lakini ninyi munawazarau wamasikini! Watajiri si ndio wale wanaowagandamiza ninyi na kuwashitaki kwenye tribinali?


Macho yao yanajaa uzinzi. Wao hawachoki kufanya zambi. Wanavuta watu wasiokamilika. Wanatawaliwa na tamaa za kupata mali. Watu hao wamelaaniwa!


Wanawaahidi watu wengine kwamba watakuwa huru ijapokuwa wao wenyewe ni watumwa wa upotovu. Kwa maana kila mutu ni mutumwa wa jambo lolote linalomutawala.


Mbele ya yote, mujue kwamba katika siku za mwisho kutakuja watu watakaoishi kufuatana na tamaa zao wenyewe. Watawachekelea ninyi


Watu hawa wanaendelea kunungunika na kuteta wengine. Wanaishi kufuatana na tamaa zao mbaya. Wanasema maneno ya majivuno na kujipendekeza kwa watu kusudi wapate faida toka kwao.


Wao waliwaambia: “Katika siku za mwisho, kutakuja watu watakaowachekelea, wakiishi kwa kufuata tamaa zao mbaya.”


Kisha yule nyama mukubwa wa pili akapewa uwezo wa kupuliza pumzi ya uzima ndani ya sanamu ya yule nyama mukubwa wa kwanza kusudi sanamu ile ipate kusema na kuweza kuua watu wasioiabudu.


Na hakukukuwa mutu aliyeweza kununua wala kuuzisha kitu pasipo kuwa na chapa ya jina la nyama yule au tarakimu zinazolingana na herufi za jina lile.


Watu hawa walimwanga damu ya watu wako na ya manabii wako, kwa sababu hiyo sasa umewakunywesha damu, nao wanastahili kutendewa vile!”


Nikaona kwamba yule mwanamuke amelewa kwa damu ya watu wa Mungu na ya watu waliouawa kwa sababu ya ushuhuda wao kwa ajili ya Yesu. Wakati nilipomwona nikashangaa sana.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ